Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, December 3, 2013

CHANONGO AIBEBA STARS CHALLENGE


chanongo_7cb80.jpg
Beki wa Somalia, Aden Hussein Ibrahim akimpitia mfungaji wa bao pekee la Stars, Haroun Chanongo Uwanja wa Nyayo leo. CHINI; Ramadhani Singano kulia na Frank Domayo kushoto wakimpongeza Chanongo katikati kwa kufunga bao hilo.
Na Mahmoud Zubeiry, Nairobi
BAO pekee la Haroun Athumani Chanongo dakika ya 57 limetosha kuipa Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Somalia mchana wa leo katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
Kwa matokeo hayo, Stars imetimiza pointi nne baada ya awali kutoa sare ya 1-1 na Zambia katika mchezo wake wa kwanza na mustakabali wake wa kuingia Robo Fainali utategemea matokeo ya mechi za mwisho za kundi hilo.
Katika mchezo wa leo, Stars ilikuwa inaanza vizuri kutokea nyuma, lakini wanapofika kwenye eneo la wapinzani wanaharibu, ama kwa kupeana pasi mbovu au kupokonywa mipira kirahisi.
Na hakukuwa na uelewano kabisa baina ya washambuliaji wa Stars, Elias Maguri, Amri Kiemba na Mrisho Ngassa hali ambayo ilifanya mabeki wa Somalia wacheze kwa uhuru zaidi.
Somalia walicheza vizuri kipindi cha kwanza na kukosa mabao mawili ya wazi, kutokana na juhudi za kipa Ivo Mapunda kuokoa hatari zote.


No comments:

Post a Comment