Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, December 3, 2013

TRA yakamata shehena ya pombe kali aina ya viroba mkoani Kagera.


 Kikosi  maalumu cha doria ya mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoani Kagera kimenasa shehena ya pombe kali aina ya viroba yenye thamani ya shilingi milioni 200 zinazoingizwa nchini kinyemela toka nchi jirani ya Uganda ikiwa ni siku chache baada ya mamlaka ya chakula na dawa nchin TFDA kanda ya ziwa itangaze tishio la afya kwa watumiaji wa viroba hivyo .
Akizungumzia tukio hilo meneja wa mamlaka ya mapato mkoani Kagera Bw. Leonard Shija pamoja na kueleza uimara wa kikosi chake cha doria amesema mkoa huo wenye vituo nane vya kuvukia kwenda nchi tatu za uganda, rwanda na burundi umekuwa na changamoto ya njia nyingi pamoja njia ya maji kupitia ziwa victoria na hivyo kuihitaji msaada wa taasisi zingine pamoja jamii kwa kutoa taarifa kwa manufaa ya nchi na watu wake.
Hata hivyo afisa forodha Bw. Mayela Baluhi na mwelimishaji elimu kwa umma TRA mkoani Kagera Bw. Lutufyo Mtafya wamesema operesheni hiyo walioielezea kuwa ya kudumu katika udhibiti wa magendo mkoani humo wamesema imefanikiwa kudhibiti uiungizaji bidhaa holela na ukwepaji kodi wakati wa kuvusha katika vituo vya Mtukula, Mulongo, Rusumo, Kabanga,Murusagamba na Kanyigo huku njia za panya zikibakia kuwa changamoto kubwa inayohitaji elimu ya uzalendo wa kudhibiti magendo nchini.
Naye mkaguzi wa chakula na kaimu meneja wa mamlaka ya chakula na dawa nchini TFDA kanda ya ziwa Bi. Nuru Mwasulama pamoja na kueleza viroba hivyo aina ya Raider, Empire na Signature kutokuwa na vibari vya kuingizwa nchini amesistiza kuwa na uwezekano wa kuathiri afya za binadamu moja kwa moja au kwa muda mrefu huku akieleza jitihada za mamlaka hiyo katika udhibiti wake kuanzia mipakani na ndani ya ukanda huo ambao umeonekana kuwa soko lake kuu.chanzo ITV


No comments:

Post a Comment