Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, December 3, 2013

Wakandarasi wasiokuwa na uwezo watakiwa kutosaini mikataba.


 Wizara ya ujenzi imewatahadharisha na kuwaonya wakandarasi wasio na uwezo wanaoingia mikataba na serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara kutotia saini mikataba hiyo kwa kuwa hawatavumilika.
Hayo yamesemwa na waziri wa ujenzi Dakt  John Magufuli wakati wa utiaji saini mikataba ya kutengeneza barabara itakayounganisha kipande cha kutoka Capetown hadi Kairo kilichokuwa kimebakia kwa upande wa Tanzania itakayopitia mikoa ya Dodoma na Manyara ambapo amewatahadharisha wakandarasi hao kutosaini mikataba hiyo kama hawana uhakika wa uwezo wao wa kujenga barabara hizo kwa muda uliopangwa.
Aidha Dkt Magufulu ameongeza kuwa serikali haitayavumilia magari yote yatakayozidisha uzito kwa kisingizia chochote kwani barabara hizo zinatengenezwa kwa kiasi kikubwa cha fedha ambazo nyingi ni za walipa kodi pamoja na mikopo kutoka sehemu mbalimbali.
Awali mtendaji mkuu wa Tanroads mhandisi Patrick Mfugare amesema wametumia taratibu zote katika kuwapata wakandarasi watakaochukua miradi hiyo kwa lengo la kuepuka wakandarasi wasiokuwa na uwezo ambao wengi wamekuwa wakiiletea serikali hasara sambamba na kuchelewesha kukamilika kwa miradi husika.
Katika hafla hiyo pia ilihudhuriwa na baadhi ya wabunge wa maeneo yote ambayo ujenzi huo utapitia ambao mbali na kuelezea kufurahishwa na hatua hiyo wamesema barabara hizo zikimalizika zitasaidia sana hasa kwa upande wa biashara sambamba na kupunguza gharama za usafirishaji.chanzoITV


No comments:

Post a Comment