Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 9, 2014

MISS VENEZUELA (2004) MONICA SPEAR AUAWA KWA KUPIGWA RISASI

Mshindi wa taji la urembo wa Venezuela mwaka 2004 (Miss Venezuela 2004) Monica Spear ameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi jumatatu, January 6.
Kwa mujibu wa The Associated Press, Majambazi hao pia walimuua kwa risasi mumewe Henry Thomas Berry aliyekuwa naye kwenye gari, na kumjeruhi mguuni mtoto wao wa kike mwenye umri wa miaka 5 anayefahamika kwa jina la Maya.  
Ripoti zilizotolewa na maafisa usalama wa Venezuela zinadai kuwa Monica ambaye pia ni muigizaji maarufu wa tamthilia (Soup-Opera), alikuwa na mumewe na mwanae huyo wakitoka mapumzikoni na kurudi Caracas, lakini bahati mbaya gari lao lilipata pancha hivyo wakalazimika kupaki pembeni ya barabara.
Majambazi walitumia nafasi hiyo kuwavamia, lakini Monica na mumewe walijifungia kwenye gari na kufunga milango ya gari wakiwa na mtoto wao ili kujinusuru.
Majambazi hao walianza kufyatua risasi. Director wa upelelezi wa Polisi wa Venezuela, Jose Gregorio amesema takribani risasi sita zilifyatuliwa na majambazi hao, na kwamba mtoto Maya anaendelea vizuri na matibabu.  
Monica Spear aliwahi kuzing’arisha tamthilia nyingi ikiwa ni pamoja na tamthilia maarufu ya ‘Pasion Prohibida’.

No comments:

Post a Comment