Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 30, 2014

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI DR SHUKURU KAWAMBWA AMESEMA CHANGAMOTO YA UPUNGUFU WA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI INAWEZA KUCHUKUA MIAKA 13 KUTATULIWA KUTOKANA NA UWEZO MDOGO WA SERIKALI KATIKA KUFUNDISHA WALIMU WAPYA KILA MWAKA

.

Aidha Dr Kawambwa amesema mahitaji ya walimu wa masomo ya sayansi ni walimu 26,000, lakini serikali inauwezo wa kutoa mafunzo kwa walimu 2100 wa fani hiyo muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Waziri Kawambwa  ametoa kauli hiyo  wakati akizindua mradi wa kompyuta ndogo za mkononi kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Wama Nakayama iliyopo wilayani Rufiji, mradi unaoratibiwa na Taasisi ya Opportunity Education ya Marekani.
Sanjari na hayo Dr Kawambwa amesema serikali ipo kwenye mkakati wa kujipanga kutumia teknolojia ili kuwezesha wanafunzi kujifunza mambo mengine licha ya idadi ndogo ya walimu iliyopo.

No comments:

Post a Comment