Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, March 11, 2014

KUTOKA BUNGE LA KATIBA LEO::MAMBO MAWILI MAKUU YALIYOPITISHWA LEO HAYA HAPA


Wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba wapitisha kwa pamoja kanuni za kuliongoza bunge hilo. Mchungaji Mtikila awa mbogo kwa Mwenyekiti wa Muda Pandu Kificho, alalamika kutopewa nafasi ya kuzungumza.
Uchaguzi wa mwenyekiti wa kudumu kufanyika kesho saa kumi jioni, Fomu za kugombea nafasi hiyo kutolewa leo ofisi za Bunge.
MAMBO MAWILI MAKUU LEO
1 Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni amewasilisha Azimio ka Kuunga mkono Kanuni za Bunge Maalum. Wabunge wengi wameridhia Azimio hilo na sasa Rasimu ya Kanuni imepitishwa na kuwa Kanuni za abunge Maalum

 2
Mwenyekiti anatoa tangazo la uchaguzi wa Mwenyekiti wa kudumu. Kwamba uchaguzi utafanyika Kesho saa 10 jioni na kwamba fomu zinapatikana kwenye ofisi za Katibu wa Bunge na wa Baraza la wawakilishi. Kuhusu nafasi ya Makamu Mwenyekiti Mwenÿekiti Kificho anasema kuwa utaratibu wa uchaguzi wa nafasi hiyo utatokana na matokeo ya uchaguzi wa Mwenyekiti

No comments:

Post a Comment