WAGONGA
nyundo wa Mbeya, klabu ya Mbeya City wameibuka na ushindi wa mabao 3-1
dhidi ya maafande wa Rhino Rangers katika mchezo wa ligi kuu soka
Tanzania bara ndani ya dimba lao la Sokoine jijini Mbeya.
Mbeya
City sasa imetimiza pointi 39, moja zaidi ya Yanga SC inayoshuka kwa
nafasi moja hadi ya tatu, baada ya kucheza mechi 21. Yanga imecheza
mechi 17.
Mabao ya Mbeya City leo yamefungwa
na Saad Kipanga mawili dakika za nane na 24 na lingine Deus Kaseke
dakika ya 34, wakati Yohana Maurice alijifunga dakika ya pili kuipatia
Rhino bao la kuongoza.
Baada
ya kumalizika kwa mchezo huo, afisa habari wa Mbeya City, Fredy Jackson
amesema kuwa mchezo ulikuwa mgumu sana kwani Rhino waliingia uwanjani
kwa lengo la kutafuta pointi tatu.
“Rhino
wameonesha upinzani mkubwa sana katika mchezo wa leo. Walidhamiria sana
kupata ushindi, lakini ubora wa wachezaji wetu umetusaidia”. Alisema
Fredy.
No comments:
Post a Comment