Wawakilishi
pekee wa Tanzania kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika Young
Africans Sports Club leo usiku wamefanya mazoezi ya mwisho katika
Uwanja wa El Max Haras El Hodod jijini Alexandria tayari kwa mchezo
marudiano kati ya mabingwa watetezi Al Ahly.
Kikosi cha Young Africans kilichowasili mchana wa leo jijni
Alexandria kikitokea jijini Cairo kimefanya mazoezi katika uwanja huo
utakaotumika kwa ajili ya mchezo wa kesho, huku morali ya wachezaji
kuelekea mchezo huo ikiwa ni ya hali ya juu sana.
Wachezaji 20
waliopo Alexandria wamefanya mazoezi chini ya makocha Hans Van der
Pluijm, Charles Mkwasa pamoja na kocha wa makipa Juma Pondamali
anayewanoa magolikipa na kuhakikisha wanaendelea kuwa fit kwa ajili ya
mchezo huo.
Kesho kikosi cha mdachi Hans kitaingia uwanjani kikiwa
na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Nadir Haroub
"Cannavaro" katika mchezo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es
salaam na kuhakikisha kinapata ushindi na kusonga mbele katika hatua
inayofuata.
Kuelekea mchezo wa kesho ambao utaonyesha na televison
zaidi ya 8 za nchini Misri, maandalizi yote yameshakamlika na katika
kikao cha maandalizi ya mechi kamisaa ameendelea kusisitiza kuwa mchezo
hautakua na mashabiki wa aina yoyote.
Wachezaji waliopo nchini Misri na kufanya mazoezi ya mwisho leo jioni ni"
Magolikipa: All Mustafa "Barthez", Juma Kaseja, Deogratias Munish "Dida"
Walinzi: Juma Abdul, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, David Luhende, Kelvin Yondani "Cotton", Nadir Haroub "Cannavaro"
Viungo: Haruna Niyonzima, Saimon Msuva, Athuman Idd "Chuji", Frank Domayo "Chumvi", Nizar Khalfani
Washambuliaji: Mrisho Ngasa, Said Bahanuzi, Emmanuel Okwi, Hamis Kizza, Jerson Tegete na Didier Kavumbagu
Mechi
itachezwa kuanzia majira ya saa 1kamili kwa saa za Misri sawa na saa 2
usiku kwa saa za Afrika Mashariki, na kesho wapenzi, wadau na wanachama
wa Young Africans watapatiwa link ya kuweza kutazama mchezo huo moja kwa
moja kwa kutumia internet.
Mungu Ibariki Young Africans, Mungu Ibariki Tanzania
BENKI YA NMB YACHANGIA VIFAA VYENYE THAMANI YA MILIONI 60 KWA SHULE TANO ZA
MSINGI WILAYA YA MUHEZA
-
Na Oscar Assenga, Muheza
BENKI ya NMB nchini imetoa imechangia vifaa vyenye thamani ya Milioni 60
kwa ajili ya kuboresha mazingira ya elimu kwa shul...
3 hours ago
No comments:
Post a Comment