Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, April 4, 2014

WAKAZI WA SUMBAWANGA VIJIJIJINI WAVUTIWA NA UTENDAJI KAZI WA KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA.!

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na baadhi ya Waalimu wa shule ya sekondari Ilemba,Sumbawanga Vijijini,alipokwenda kukagua ujenzi wa bweni la wasichana wa shule hiyo,iliopo nje ya kilometa 104 kutoka Sumbawanga Mjini.
Sehemu ya bweni hilo la Wasichana,ujenzi wake ukiendelea.
Ndugu Kinana akipokea taarifa ya Shule ya Sekondari ya Ilemba kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Sumbawanga Vijijini,Bwa.Abeid Missana.Shule hiyo yenye jumla ya wanafunzi 237 inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo tatizo la uhaba wa walimu wa masomo ya Sayansi,Nyumba za walimu na idadi ya waalimu waliopo.
Kinana akishiriki ujenzi wa jengo hilo la Bweni la wasichana shule ya sekondari ya Ilemba.
Katibu Mkuu wa CCM,akiwa ameongozana na baadhi ya Viongozi wa Chama Wilaya na Mkoa wakielekea kukagua na kujionea maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya,kilichopo kata ya Ilemba;Sumbawanga Vijijini
Kinana akipitishwa kukagua ujenzi wa zahanati hiyo na Ofisa Mtendaji wa Kijiji,Kata ya  Ilemba,Bwa.Desdei Kayola (pichani kati)
Muonekano wa ujenzi wa kituo hicho cha afya,kata ya Ilemba ambacho kikikamilika kitaokoa maisha ya idadi kubwa ya watu,ambayo inapotea kutokana na uduni wa huduma ya afya iliyopo sasa,hivyo kituo hicho kitatatua changamoto zilizopo za huduma ya afya.

 
Kinana akikagua ujenzi wa kituo cha Polisi kata Ilemba,Sumbawanga vijijini.
 Kinana akishiriki ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Kata ya Ilemba, Sumbawanga Vijijini. Ameahidi kutoa mifuko 50 ya saruji na bati 50 kumalizia ujenzi wa kituo hicho

Wananchi wa kata ya Ilemba wakiwa na mabango Wakimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM,ndugu Kinana
Wananchi wa Kijiji cha Ilemba wakifuatilia mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Ilemba.
Baadhi ya Wanachama wapya wapato 300 kutoka kata ya Ilemba, waliojiunga na chama cha CCM,wakila kiapo mara baada ya kukabidhiwa kadi za chama hicho na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia maelfu ya wananchi, katika kijiji cha Ilemba, kata ya Ilemba, alipohutubia wananchi katika kata hiyo akiwa katika  ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika wilaya Sumbawanga Vijijini mkoani Rukwa.
Wananchi wa kijiji cha Ilango,Kata ya Ilemba,Sumbawanga vijijini wakimpokea katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kwa aina yake alipokuwa akiwasili kijijini hapo ambapo pia aliongea na kuwasikiliza matatizo yao ikiwemo na kuyafanyia kazi.

No comments:

Post a Comment