Pages

Monday, December 15, 2014

MGOMBEA CHADEMA MTAA WA MIGOMBANI SEGEREA, JAPHET KEMBO AWAGARAGAZA WAPINZANI WAKE KWA KUPATA KURA 510

Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani Kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema) Japhet Kembo akifurahia huku akipongezwa na wanachama na wapenzi wa Chadema mara baada ya kuibuka mshindi wa Kiti cha Mwenyekiti kwa Kupata Kura 510 huku CCM wakiwa wamepata kura 215 na NCCR kupata kura 205
 Mawakala wa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Migombani wakihesabu kura ambapo sanduku hilo ndio lilikuwa sanduku la mwisho kuhesabiwa katika Kituo cha Kupigia kura cha Migombani ambao wakazi wa Mtaa wa Migombani walikuwa wakisubiria matokeo


 Askari Polisi wakiwa katika kituo cha Kupigia Kura cha Migombani kwaajili ya kuimarisha ulinzi na mpaka zoezi la kuhesabu kura likimalizika kwa Mgombea wa Chadema kuibuka Mshindi hakuna fujo zilizotokea.
Baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Migombani Wakisubiria Matokeo ya Uchaguzi wa Serikali ya Mtaa wa Migombani ambapo mpaka matokeo yanatangazwa Chadema iliibuka na Kura 510, CCM ikiwa imepata kura 215 na NCCR wakiwa na kura 205.
Baadhi ya wapita njia nao ilibidi wasimame maana uchaguzi huu ulivuta hisia za watu wengi kutokana na hali iliyoonyeshwa na wakazi wa mtaa huo kukaa mpaka dakika za mwisho
 Msimamizi wa Uchaguzi katika Kituo cha Kupigia Kura cha Migombani akitangaza Mshindi wa Uchaguzi huo uliomalizika kwa Mgombea wa Chadema akiwa ameibuka Mshindi kwa Kupata Kura 510 huku wapinzani wake wakiwa na Kura 215 za CCM na Kura 205 za NCCR
 Wakazi wa Mtaa wa Migombani wakishangilia ushindi mara baada ya Mgombea wa Chadema Kutangazwa Mshindi wa Kiti cha Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani
 Wakazi wakishangilia kwa Ushindi,
 Mgombea wa Nafasi ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani Japhet Kembo (Kushoto aliyenyoosha mkono) akipongezwa na wakazi wa Mtaa wa Migombani kwa kuibuka Mshindi wa uchaguzi
Wakazi wa Mtaa wa Migombani Segerea wakishangilia mara baada ya mgombea wao kuibuka mshindi katika kinyanganyiro hiko.Picha Zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

No comments:

Post a Comment