Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, March 5, 2015

PICHA 20;;; TUKIO LA MVUA YA MAWE MAKUBWA ILIYOUA WATU WENGI HUKO MWAKATA-KAHAMA



Mwananchi akiwa amebeba moja ya barafu la mvua,yaliyokuwa yanadondoshwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia leo katika Kata ya Mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Mawe hayo ya mvua yanadaiwa kuwa na ukubwa wa ndoo ya lita 10,na yalikuwa yamezagaa katika kijiji hicho baada ya mvua kukatika.Pichani ni barafu ikiwa imeanza kuyeyuka




Miili ya watu 7 wa familia moja waliokufa katika tukio hilo

Watu 38  wamefariki dunia na wengine 82 wamejeruhiwa baada ya kuangukiwa na nyumba kutokana na mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na upepo kunyesha usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Mwakata Kata ya Mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga.



Mbuzi wakiwa wamekufa


Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi ya wilaya ya Kahama, ambaye ni mkuu wa wilaya hiyo Benson Mpesya(mwenye suti) amesema kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya itakaa kabla ya kamati ya mkoa ili kupata taarifa zitakazoisaidia serikali kuanza kutoa misaada. eneo la tukio
 

















Picha zote na Faraji Mfinanga,Shabani Alley na Mohab Dominic-Malunde1 blog Kahama



No comments:

Post a Comment