Na Joseph Ngilisho
Unyama ulioje! Wanawake wanne wanaojiita Kundi la ‘Boko
Aramu, hivi karibuni wamemteka msichana mmoja mrembo aitwaye Marry kisha
kumfanyia kitu mbaya ikiwa ni pamoja na kumdhuru sehemu zake za siri.
Marry akiwa katika Hospitali ya Mount Meru, baada ya
kunusurika kuchinjwa.
Sikia simulizi ya Marry
Akizungumza kwa tabu akiwa katika Hospitali ya Mount Meru,
Marry ambaye anamiliki saluni ya kike alisema, chanzo cha kufanyiwa hivyo ni
wivu wa mapenzi huku akimtaja rafiki yake wa karibu aitwaye Maurin kuhusika.
Alisema, siku ya tukio akiwa ndani ya saluni yake alifika
Maurin na kumtaka aende kwenye chumba chake kuna jambo akamsaidie lakini
alipofika huko akashangaa anataitiwa.
“Ilikuwa saa mbili usiku, alikuja Maurin na kuniomba niende
katika chumba chake, nilipofika tu mlangoni kwake akanisukumia kitandani, mara
nikaona kundi la wanawake likinivamia na kuanza kunishambulia.
“Walinipiga sana, baadaye walinivua nguo zote na kunilaza
kitandani kisha mmoja akanifanyika kitendo cha kikatili ambacho siwezi hata
kukisimulia.
Baadhi ya ndugu wa Marry wakiwa katika kituo cha polisi.
Niliumia sana, nikapiga kelele sana lakini hawakuniachia,”
alisema Marry na kuongeza:
“Walizidi kunikandamiza, nahisi lengo lao ilikuwa ni kuniua.
Mara mwanamke mmoja akaniuliza kwa nini natembea na bwana wa Maurin.
Nikashangaa kusikia maneno hayo. Nikawaambia Maurin ni rafiki yangu na wala
huyo bwana wake simjui. Basi wakazidi kunipiga.
“Mmoja akachukua kisu na kuniwekea shingoni, mwingine akachukua
kichupa ambacho nahisi kilikuwa na tindikali, ikabidi nijilazimishe kuamka na
kuwapigia magoti wasiniue.“Wakakubali kunisamahe lakini wakadai niwalipe
gharama zao kwani wametoka Dar kuja kuniua. Nikawaambia sikuwa na fedha,
wakaitana pembeni kisha wakaondoka na kuniacha pale nikiwa na maumivu.
“Walipoondoka tu nikaanza kupiga kelele na ndipo watu
walipokuja kunipa msaada kisha tukaenda kutoa taarifa katika kituo kikuu cha
polisi na kufungua jalada la kesi lenye namba AR /RB /3717/2015,” alisema
Marry.
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Edward
Balele alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa mpaka sasa jeshi
hilo linawashikilia wanawake wawili kati ya wanne waliohusika kumtendea unyama
dada huyo.CHANZO GPL
No comments:
Post a Comment