Karibu watu 19 wamejeruhiwa baada ya kutokea mlipuko uliosababisha majengo mawili kuanguka katika Jiji la New York. Hadi jana mchana majira ya Marekani zaidi ya zimamoto 200 walikuwa wakipambana na moto wa mlipuko huo, ambao uliathiri majengo manne.
Vikosi vya zimamoto vikipambana na moto
Meya wa Jiji la New York, Bill de Blasio amesema hakuna ripoti ya mtu aliyepotea, hata hivyo amekiri hali ni tete. Maafisa wa Jiji hilo wanaamini kulikuwa na kazi ikiendelea katika majengo hayo yenye mfumo wa gesi kabla ya kulipuka.
No comments:
Post a Comment