Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, December 1, 2012

‘TUTARUDISHA KODI YA PANGO YA SHARO MILIONEA’

 

WAMILIKI wa nyumba aliyokuwa akiishi msanii wa Komedi, Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’ wamesema watarudisha kiasi chote cha fedha ya kodi ya pango kilichotolewa na nyota huyo.
Wakiongea na Saluti5 jana, wamiliki hao wameahidi kukabidhi pesa zote za kodi ya pango zilizokuwa zimelipwa na Sharo, siku vitakapokuwa vinatolewa vyombo.
“Hatuwezi kuzuia hela iliyotolewa na Sharo kama kodi ya pango kwa sababu kitendo hicho ni sawa na dhuluma ambayo ni kosa kwa mujibu wa dini yetu ya Kikristo,” walisema wamiliki hao.
Walisema kuwa, watairudisha kodi hiyo kwasababu Sharo alihamia kwenye nyumba yao takriban wiki moja tu kabla ya ajali iliyosababisha mauti kumfika.
SOURCE SALUTI5

No comments:

Post a Comment