Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, February 3, 2015

Kaburi la kamanda wa LRA lapatikana

 mwanajeshi wa LRA
Jeshi nchini Uganda linasema kuwa limegundua mabaki ya kamanda wa cheo cha juu wa kundi la waasi wa Lords Resistance Army LRA.
Okot Odhiambo ambaye alikuwa mmoja wa makamanda watano waliokuwa wakitafutwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC huenda aliuawa kwenye mapigano mwaka 2013.
Uchunguzi wa DNA unafanywa kuthibitisha mabaki hayo.
Kiongozi wa LRA Jospeh Kony
Kamanda mwingine wa LRA Dominic Ongwen 


alifikiswa mbele ya mahakama ya ICC wiki iliyopita.

Hata hivyo kiongozi wa LRA Joseph Kony bado yuko mafichoni.

No comments:

Post a Comment