Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sports news

NSA JOB AITOSA VILLA - AENDA SWEDEN KUJARIBU ZALI


 
MSHAMBULIAJI wa Villa Squad, Nsa Job, amepata ulaji wa kwenda kufanya majaribio Sweden kutokana na kiwango chake kuwa juu kwa sasa.
 Mwenyekiti wa Villa, Uledi Ramadhani, alisema Nsa alimwambia kuwa anatarajia kuondoka nchini mara baada ya ligi kumalizika kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.
Alisema awali Nsa alimwambia anaenda Ulaya bila kuwatajia sehemu aendayo lakini watu wake wa karibu wakamwambia anakwenda Sweden ambako ametafutiwa timu na wakala wake.
“Nsa aliniambia anatarajia kwenda Ulaya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa mara baada ya ligi kumalizika ingawa hakuniambia ni nchi gani anaenda, ila wenzake waliniambia amepata timu Sweden.
“Binafsi namuunga mkono kwa hilo kwa kuwa sisi tunapenda maendeleo, hivyo tutafurahi tukiona amefanikiwa kwa kuwa ni njia mojawapo ya kuitangaza Villa,” alisema Uledi.
Nsa alipotafutwa kuzungumzia mpango huo alikiri: “Kweli naondoka kati ya tarehe sita au saba mwezi wa tano, nakwenda Sweden kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.”
Nsa aliyejiunga na Villa Julai, mwaka jana akitokea Yanga, amefanikiwa kuonyesha uwezo mkubwa katika michezo ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Bara akiwa amefunga mabao kumi mpaka sasa.

EDEN HAZARD AZIANGALIA UNITED NA CITY ZIKICHUANA - MASAA 24 BAADA YA KUIADHIBU PSG

Eden Hazard alikuwa mmoja ya watu maarufu walioenda kuangalia mechi katika ya mahasimu wawili wa jiji la Manchester.

Timu hizi mbili zote zimekuwa zikihusishwa na kumsajili kinda huyo mwenye kipaji cha hatari akiwa na miaka 21,  hivyo kusababisha vita nyingine baina ya rivals hawa.

Roberto Mancini wikiendi iliyopita aliongeza joto la vita hiyo kwa kumwambia Hazard kwamba City ndio mahala panapomfaa.

Boss wa United Sir Alex Ferguson pia amethibitisha kuwa anavutiwa na Hazard na alienda kumuangalia nchini Ufaransa.

Arsenal na Tottenham wote nao wapo katika kuwinda saini ya kinda hilo.

Hazard alienda nchini Uingereza jijini Manchester kwa ajili ya kuangalia derby masaa 24 baada ya kufunga goli moja na kutengeneza lingine katika ushindi wa Lille wa 2-1 dhidi ya Pars Saint Germain.


KOCHA MPYA WA ENGLAND: NITAONGEA NA RIO NA TERRY, ROONEY ATAKUWEMO KATIKA KIKOSI CHANGU - SHEARER ATAJWA KUWA MSAIDIZI WAKE



Kocha mpya wa England
Kocha mpya wa England Roy Hodgson ataongea na John Terry na Rio Ferdinand kwa matumaini ya kuwachukua wachezaji wote wawili katika michuano ya EURO 2012.

Kazi kubwa ya kwanza kwa Hodgson ni kunitibu majeraha ya uhusiano mbovu uliopo baina ya wachezaji  katika chumba cha kubadilishia nguo uliotokea baada ya Terry kutuhumiwa kumtolea maneno ya kibaguzi Antoni Ferdinand - ambaye ni mdogo wake Rio. mwezi October mwaka jana.

Terry na Ferdinand wanabakia kuwa mabeki wenye ushirikiano mzuri katika timu ya taifa na wakati akitangazwa rasmi katika uwanja wa Wembley, Roy alikaririwa akisema: "Itabidi niongee na John na Rio, natumaini tutakutana uso kwa uso, na kujua nini suluhisho.

"Kwa sasa siwezi kusema chochote  mpaka nitakapogundua kiundani mahusiano yao yapoje - na nafikiri sitoongeea na wao tu, nitaongea na wachezaji wote wakubwa ndani ya kikosi."

Hodgson, ambaye amesema kwamba atamchagua Wayne Rooney katika kikosi cha wachezaji 23 - ambacho atakitangaza muda mfupi baada ya msimu kuisha - bado hajaamua kuhusu wasaidizi wake.

Lakini inaaminika atamchagua msaidizi mmoja, ingawa bado hajaongea na kocha wa England chini ya miaka 21 na kocha wa timu ya Uingereza ya Olympic Staurt Pearce kuhusu jinsi ya kuhusika kwake katika EURO 2012.
Alan Shearer

Mtu anayetajwa sana kuweza kuchaguliwa kama msaidizi wa Roy ni Alan Shearer ambaye anatajwa kuwa na mahusiano ya karibu sana na Hodgson. 
 
 

CRISTIANO RONALDO, BENZEMA NA HIGUAIN WAVUNJA REKODI YA LIGI YA HISPANIA KWA MAGOLI




Cristiano Ronaldo, Benzema na Higuain wametengeneza historia mpya kwenye La Liga baada ya kila mmoja magoli 20 au zaidi katika ligi hiyo ndani ya msimu mmoja. Haijawahi kutokea katika historia ya ligi hiyo kwa wachezaji wa timu moja kufanikiwa kufanya hivi.


GOALS THIS SEASON
PLAYER LA LIGA UCL COPA S. S. CUP TOTAL
Ronaldo 43 10 3 1  57
Benzema 20  7 3 1  31
Higuain 21  3 1 -  25
TOTAL 84 20 7 2 113

Washambuliaji hawa watatu ndio wanatengeneza safu kali ya ushambuliaji kwenye La Liga wakiwa wamefunga mabao 113 katika msimu mmoja, Ronaldo akiwa akafunga mabao 57 - magoli mengi zaidi katika kalbu hiyo.

TOP SCORING REAL MADRID ATTACKING TRIOS
Season Players (goals) Total
2011/12 Cristiano (57), Benzema (31), Higuain (25) 113
1959/60 Puskas (49), Di Stefano (24), Pepillo (22) 95
2010/11 Cristiano (53), Benzema (26), Higuain (13) 92
1960/61 Puskas (41), Di Stefano (29), Del Sol (18) 88
1961/62 Puskas (40), Di Stefano (22), Tejada (20) 82
1932/33 Olivares (39), Regueiro (24), Hilario (19) 82
1956/57 Di Stefano (43), Joseito (17), Mateos (17) 77
1988/89 H. Sanchez (37), Butragueño (22), Michel (15) 74
1957/58 Di Stefano (36), Rial (22), Marsal (15) 73
1958/59 Di Stefano (34), Puskas (25), Rial (13) 72

No comments:

Post a Comment