Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, August 23, 2012

Bibi Veronica Mpangala ndiye mshindi wa Bibi Bomba kupitia Clouds TV

Bibi Veronica Mpangala akikabidhiwa mfano wa hundi ya Tsh mil 5 baada kuwa mshindi wa kwanza.
Lile shindano la Bibi Bomba lilokuwa likiendeshwa na Clouds TV limefikia kilele chake dakika chache zilizopita na Bibi Veronica Mpangala kuibuka mshindi kwa kuwazidi wenzake kwa mbali sana kama graph inavyoonesha kwenye picha zinazo endelea. Bi Veronica amejishindia Tsh 5,000,000/= pamoja na zawadi nyingine. Nafasi ya pili imeshikwa na Anna Said a.k.a Mzee wa Dongo na kupata Tsh. 3,000,000/= wakati nafasi ya tatu ikishikwa na Bi. Nasra Mohamed ambaye ameshinda Tsh. 1,500,000. Washiriki wengine walioingia kwenye 8 bora walijipatia zawadi ambazo hazikutajwa.
Ona Bibi Veronica alivyo wakimbiza washiriki wenzake
Huyu ni mshindi wa pili Bibi Anna Said a.k.a Mzee wa Dongo aliye jishindia Tsh 3,000,000
Nasra Mohamed ,mshindi wa tatu wa Bibi Bomba akikabidhiwa mfano wa hundi wa sh. 1,500,000/ na Staa wa Filamu za Kibongo JB
source tulonge

No comments:

Post a Comment