wanafunzi wa shule za msingi mjini Iringa wakienda shule na senene |
Gari lenye namba za usajili T 356 BXK likiwa limebeba senene kupeleka sokoni Iringa kuuza |
Kijana akiwa amebeba magunia ya Senene katika mkokoteni akielekea kusaka wateja |
Senene wakiwa wamezagaa katika jengo la Asas |
Mvua
kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia leo katika mji wa Iringa
imeshusha neema kwa wakazi wa mji wa Iringa ambao ni wapenzi wa
Senene baada ya baadhi ya wamiliki wa nyumba kudaiwa kuwazuia
wapangaji wao kuokota senene katika nyumba zao huku walimu pamoja na
watumishi wa umma wakichelewa kuingia makazini kutokana na zoezi
la kuokota senene hao.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi katika shule mbali mbali za Manispaa ya Iringa asubuhi ya jana umebaini kuwa idadi kubwa ya wanafunzi na walimu wao walionekana katika maeneo ya shule hizo wakikusanya senene huku baadhi ya wazazi wakilalamikia baadhi ya walimu kuwapa adhabu ya kukamata senene kwa wanafunzi waliochelewa kufika shule.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi katika shule mbali mbali za Manispaa ya Iringa asubuhi ya jana umebaini kuwa idadi kubwa ya wanafunzi na walimu wao walionekana katika maeneo ya shule hizo wakikusanya senene huku baadhi ya wazazi wakilalamikia baadhi ya walimu kuwapa adhabu ya kukamata senene kwa wanafunzi waliochelewa kufika shule.
Mmoja
kati ya wazazi ambaye alijitambulisha kwa jina la Jackson Ndelwa
alisema kuwa anashangazwa na utaratibu wa walimu wa shule mbali
mbali za msingi katika Manispaa ya Iringa kuwaacha wanafunzi
wakiendelea kukamata senene katika maeneo ya shule hadi mida
ya saa 4 asubuhi wakati kwa kawaida muda huo wanafunzi wanapaswa
kuwa madarasani .
Hivyo aliuomba uongozi wa elimu katika Manispaa ya Iringa
kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi na walimu wao kwa siku ya jana na
iwapo itabainika kuwa wanafunzi hawakuingia madarasani kwa ajili ya
kufanya shughuli za kukamata senene za walimu basi walimu
waliohusika kuwapa wanafunzi adhabu ya kukamata senene wakati wa
mvua kuchukuliwa hatua kali.
Mmoja
kati ya walimu wa shule za msingi mjini Iringa ambae aliomba jina
lake na shule yake kuhifadhiwa kwa kuwa si
msemaji wa walimu mjini Iringa alisema kuwa madai ya wazazi kuhusu
wanafunzi kutumwa na walimu wao wa madarasa kuokota senene ni ya
kweli na kuwa badhi ya walimu na wanafunzi kwa muda wa asubuhi
walikuwa wakishindana kufukuza senene kama kitoweo .
Pia
alisema kwa siku ya jana hata adhabu za kawaida ambazo walimu
wamekuwa wakizitoa kwa wanafunzi wanaochelewa kama adhabu ya viboko
haikuwepo na badala yake wanafunzi waliochelewa walikuwa wakipewa
adhabu ya kukusanya senene kwa ajili ya kitoweo cha walimu na sehemu
ya senene wanafunzi wamekuwa wakipewa .
Wakati wazazi wa wanafunzi hao wakilalamikia hatua ya walimu wa
shule za msingi kuwatumia wanafunzi katika kuokota senene kwa
upande wao baadhi ya wamiliki wa nyumba katika mji wa Iringa
wamedaiwa kuwanyanyasa wapangaji wao kwa kuwazuia kuokota senene
zinazoanguka katika nyumba zao kwa madai kuwa senene hizo ni mali
ya mwenye nyumba na iwapo wanataka basi kutoka nje ya uzio wa nyumba
hizo usiku kwenda kusaka senene mitaani .
Mbali
ya wanafunzi hao na baadhi ya wamiliki wa nyumba mjini Iringa
kuonyesha kugombea senene hao badhi ya wananchi wameweza kunufaika
zaidi ya senene hao kwa kuokota magunia kwa magunia ya senene na
kuwauza kati ya shilingi 35,000 hadi 50,000 huku walinzi wa maeneo
mbali mbali ya biashara mjini hapa wakiacha malindo yao na
kukusanyika eneo la jengo la mfanyabiashara Salim Abri Asas kukusanya
senene hadi mida ya saa 7 mchana kutokana na eneo hilo kuwekwa taa
zenye mwanga mkali
zaidi.
No comments:
Post a Comment