Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, February 2, 2013

BINTI WA MIAKA 13 AFANYIWA KITCHEN PARTY.....POLISI AINGILIA KATI



 Binti huyo (kushoto) akiwa chini ya ulinzi wa polisi akitolewa ndani na kuingizwa kwenye gari

Hakuna lugha nyepesi unayoweza kuzungumza zaidi ya kusema haya ni maajabu ya mwaka 2013, kwani familia ya Masoud Kassim wa Karakata Ukonga Dar imejikuta ikiingia kwenye mgogoro wa kisheria baada ya kuamua kumfanyia ‘kitchen party’  mtoto wao wa miaka 13 aitwaye Rafia Masoud, tayari kwa ndoa.
 akiingizwa kwenye gari ambapo alipelekwa Kituo cha Polisi, Stakishari kwa mahojiano zaidi.

Tukio hilo la kusikitisha na kuhuzunisha limetokea Jumatano ya wiki iliyopita ambapo Gpl ilikuta Rafia akiwa katika sherehe hizo huku ndoa yake ikitarajiwa kufungwa leo Februari 2.
 Akina mama walikokuwa katika sherehe hiyo wakitahamaki baada ya kachero wa polisi kujitambulisha

No comments:

Post a Comment