Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, April 19, 2013

AIBUU...MWANACHUO AVULIWA NGUO NA KUPEWA KICHAPO KIKALI BAADA YA KUIBA VIATU..Angalia PICHA

 Mrembo  huyu  aliyejitambulisha  kwa  ni mwanafunzi  wa chuo  kikuu  kimojawapo mjini Iringa akilia baada ya kupokea  kichapo kutoka kwa mwanamke mfanyabiashara  eneo la Miyomboni mjini Iringa baada ya  kuiba viatu  vya mtumba na kuficha kwapani
Hapa  akimpigia  simu mpenzi  wake  ili aweze kumkomboa baada ya  kutakiwa  kulipa Tsh 50,000 kwa viatu pea mbili alizoiba .

Tukio la mrembo  huyo  kupokea  kichapo na kuvuliwa  nguo na  kupokonywa  simu yake na mikoba zaidi ya mitano  pamoja na kiasi cha TSh 15,000 ambazo alikuwa amezihifadhi limetokea  jumapili  wiki hii katika  eneo la Miyomboni mjini Iringa.

Akielezea juu ya mkasa  huo  wa aina yake  leo mfanyabiashara   huyo  mama Masawe  alisema kuwa eneo  hilo amekuwa na kawaida ya  kuibiwa  viatu katika  duka  lake la viatu  vya mtumba .....

Mama  huyu  anadai    kuwa  mbali ya  kukamatwa kwa mrembo  huyo  bado amepata  kukamata  vijana  zaidi ya  wawili watanashati ambao  wamekuwa wakifika na kujifanya wakichagua viatu na  kuishia  kuiba na kutoweka .

Binti   huyo ambaye  ni  mwanachuo   alifika  dukani hapo   na  kuanza kuchagua  viatu akijifanya  ni  mteja .....
 
Baada  ya  kuona  muuza  duka  ameangalia  pembeni, binti  huyo   alichukua  pea  moja  ya  viatu  na  kuificha  kwapani  asijue  kwamba  pembeni  kulikuwa  na  mtu  mwingine  aliyekuwa  akimwangalia....
 
Alipoaga na  kutaka  kuondoka ndipo timbwili la  kichapo  lilipoanza kwa mrembo huyo ambae aliomba asipelekwe  polisi  na  asipewe  adhabu  kubwa  kwa  kuwa   ana ujauzito  wa miezi mitatu tumboni.

Alisema  kuwa  kutokana na maombi ya mrembo huyo  kupunguziwa adhabu  hakuweza kumfikisha  polisi  zaidi ya kumpa kichapo  cha kufa mtu na kumpokonya  mali  zote alizokuwa ametoka  kuiba katika maduka ya  Miyomboni mjini hapa pamoja na  simu  yake ya kiganjani .


No comments:

Post a Comment