DSC01222
Diwani wa CHADEMA kata ya Mungaa jimbo la Singida Mashariki, Matheo Alex (wa pili kushoto aliyenyanyua mkono juu) akiwa katika chumba cha mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida akisubiri kusomewa shitaka lake la kukata kata ng’ombe sita mali ya Mary John mkazi wa kijiji cha Minyinga kata ya Mungaa.Wa pili kulia ni mtoto wa diwani Alex, Faraja na wa pili kushoto Bahati Sumbe (mwenye jacketi la njano) wameunganishwa kwenye kesi moja na diwani Alex.
DSC01237
Mwenyekiti wa CCM kijiji cha Minyinga kata ya Mungaa jimbo la Singida mashariki, John Theodore Ghumpi (wa kwaza kushoto) akimhoji mbunge Tundu Lissu, ni kwa nini anatetea wahalifu ambao amedai wamejichukulia sheria mkononi kwa kukata kata ng’ombe zake sita.Ghumpi ni mume wa Mary John.(Picha na Nathaniel Limu).