Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, June 27, 2013

HALI YAZIDI KUWA TETE KATIKA CHUO KIKUU CHA TEOFELO KISANJI, UONGOZI WA CHUO NAO WATOA TAMKO .

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji Dk.Daniel Mosses akisoma Tamko kwa Waandishi wa Habari


 Waandishi wa Habari wakiwa nje ya ofisi ya Makamu Mkuu wa Chuo kwa zaidi ya Masaa Matatu
 Waandishi wa Habari wakimsikiliza Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji Dk.Daniel Mosses akisoma Tamko kwa Waandishi wa Habari
 
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofelo kisanji wakingoja kusikia Hatima yao


Hali bado ni tete katika Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji baada ya siku moja kupita tangu Chama cha Wahadhili wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji(TEKUASA) kutangaza kutotunga mitihani ya kufungia Mhula, Uongozi wa Chuo wasimama na kukanusha Mgomo huo.
Akisoma Tamko la kukanusha uwepo wa Mgomo huo, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Daniel Mosses amesema Mitihani itafanyika kama ilivyopangwa kuanzia Julai Mosi Mwaka huu hadi Alhamisi ya Julai 11, Mwaka huu.
Hata hivyo Kaimu Mwenyekiti wa TEKUASA, Amani Sembeye,alivyopigiwa simu kuhusiana na maamuzi ya Menejiment amesema msimamo wao uko pale pale.

Ameongeza kuwa kama  kungekuwa na msimamo tofauti na walivyotoa kwa vyombo vya habari awali basi wangeitisha tena mkutano mwingine kwa ajili ya kubatilisha.

No comments:

Post a Comment