Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, June 9, 2013

MRITHI WA MARTINEZ KUPATIKANA WIKI IJAYO- WHELAN!!



Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Mwenyekiti wa klabu ya Wigan Athletic, Dave Whelan amethibitisha kuwa wiki ijayo anaanza usaili wa kupata makocha wa kuifundisha klabu hiyo na kusema kuwa muda kama huu wiki ijayo tayari timu hiyo itakuwa na kocha mpya.
Whelan amelazimika kutafuta meneja mpya baada ya aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Roberto Martinez kutimkia katika klabu ya Everton kurithi mikoba ya aliyekuwa kocha wa klabu hiyo David Moyes aliyejiunga na mabingwa wa ligi kuu nchini England, Manchester United.
Whelan ameuambia mtandao wa michezo wa Sky Sports kuwa amepata makocha 10 hadi 12 wa kuwafanyia usaili siku chache zijazo na wiki ijayo atatangaza rasmi kocha mpya wa mabingwa hao wa kombe la FA.
“Kuna maombi 50, lakini siwezi kuwafanyia usaili yote, ila nawashukuru kwa kutuma maombi”. Alisema Whelan.
Majina yanayotaja kuziba nafasi hiyo ni  Brighton’s Gus Poyet, Mike Phelan na Rene Meulensteen – wote walikuwa wasaidizi wa Ferguson,  Karl Robinson na kocha wa zamani wa Bolton na Burnley, Owen Coyle.
Hata hivyo Whelan alisema hataangalia majina, lakini atazungumza na makocha wengi na mwishoni anataka kumsainisha kocha mkubwa na haitakuwa kazi nyepesi kwake.
Vacancy: Roberto Martinez (right) quit Wigan to take over at Everton following the departure of David MoyesNafasi imebaki wazi Wigan: Roberto Martinez (kulia) ametimka  Wigan  na kujiunga na Everton ili kurithi mikoba ya David Moyes
Leaving present: Martinez departed after winning the FA Cup with Wigan but also suffered relegationKatimka baada ya kuacha taji: Martinez ametimka baada ya kushinda taji la FA
In the running: Former Manchester United coach Rene Meulensteen (left) has been linked with the Wigan jobKocha wa zamani wa  Manchester United  Rene Meulensteen (kushoto) naye ametajwa kuwania kibarua katika klabu ya Wigan 
source fullshangwe blog

No comments:

Post a Comment