Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, July 19, 2013

Jeshi la Kongo lashambulia waasi

Majeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwa kutumia helikopta yameyashambulia maeneo ya waasi karibu na upande wa mashariki mwa mji wa Goma, ikiwa siku ya tatu ya mapigano makali yaliyosabaisha wimbi la ukimbizi.
Katika barua ilitumwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambayo Shirila la habari la Reuters limepata nakala yake, Kongo imekituhumu kikosi maalumu cha Rwanda kwa kuwasaidia waasi wa M23 katika mapigano hayo. Lakini pia katika taarifa yao walinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa nchini Kongo wamekanusha madai ya Rwanda kwamba walifyatua makombora dhidi ya nchi hiyo kutoka ardhi ya Kongo Jumatatu.
Taarifa ya jeshi hilo la ulinzi wa amani lijulikalo kama MONUSCO, umesema wanajeshi wake hawajahusika na mapigano katika eneo la Goma na kwa hivyo hawawezi kuhusika katika kufyatua makombora kwenye mipaka ya Rwanda.
Malalamiko ya Rwanda
Rwanda's President Paul Kagame attends the signing ceremony of the Peace, Security and Cooperation Framework for the Democratic Republic of Congo and the Great Lakes, at the African Union headquarters in Ethiopia's capital Addis Ababa Feburary 24, 2013. A U.N .-mediated peace deal aimed at ending two decades of conflict in the east of the Democratic Republic of Congo was signed on Sunday by leaders of Africa's Great Lakes region in the Ethiopian capital Addis Ababa. REUTERS/Tiksa Negeri (ETHIOPIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST HEADSHOT) Rais Paul Kagame wa Rwanda
Katika taarifa tofauti iliyotolewa jumatatu kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Rwanda imelituhumu jeshi maalumu la ulinzi wa amani nchini Kongo kuwa linashirikiana na waasi wa Kihutu, wa kundi la FDLR, ambao wanahusishwa na mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994. Jeshi hilo jipya lina mamlaka ya kupigana na kuwanyang'anya silaha waasi katika eneo la mashariki mwa Kongo.
Mpaka sasa walinzi hao wa amani 3,000 kutoka Afrika Kusini, Tanzania na Malawi wanafanya doria lakini bado hawajajiingiza katika mapigano. Umoja wa Mataifa tayari umekwisha onya, kwamba utazuia shambulio lolote lenye kulenga Goma, mji wenye kiasi ya watu milioni moja, ambao mwezi Novemba ulitekwa na waasi kwa kipindi kifupi.
Civilians react to shell fire erupting as Congolese armed forces drive through the area of Munigi on the outskirts of Goma in the east of the Democratic Republic of the Congo on July 15, 2013. At least 130 people were killed, including 10 soldiers, in the deadliest clashes in months between troops and rebels in the restive eastern Democratic Republic of Congo, the government said on July 15. Fierce fighting broke out on July 14 outside the flashpoint city of Goma between the Congolese army and the M23 rebels, an armed group launched by Tutsi former soldiers who mutinied in April 2012. The clashes continued on July 15 between Congolese armed forces and M23 rebels, causing several thousands of people to flee. AFP PHOTO / PHIL MOORE (Photo credit should read PHIL MOORE/AFP/Getty Images) Eneo la Munigi, pembezoni mwa mji wa Goma
Mwandishi wa Reuters katika eneo la Mutaho, kiasi cha kilometa saba, kaskazini/mashariki mwa Goma amesema aliziona helikopta tatu za jeshi la Kongo zikishambulia eneo la waasi, mji wa Kibati ambao upo umbali ya kilometa 4 zaidi.
Msemaji wa Jeshi Kanali Olivier Hamuli aliliambia shirika hilo mjini Mutaho, kwamba hali hivi sasa imetulia. Akizungumzia operesheni ya asubuhi ya jana amesema walishambulia jana alfajiri lakini walijibu mapigo na kwamba lengo lao ni kuwasafisha waasi wote wa M23.
Awali Jumatatu Waasi na Majeshi ya Kongo walifyatuliana makombora karibu na kaskazini na magharibi mwa viunga vya mji wa Goma. Umoja wa mataifa unasema makombora hayo yalifika umbali wa mita 100 kutoka uwanja wa ndege wa Goma lakini hakuna hasara zozote zilizoripotiwa.

No comments:

Post a Comment