Mtuhumiwa Edwin Monyo (39) anayedaiwa kusafirisha dawa za kulevya zenye thamani ya Sh milioni 68, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashitaka hayo.
Monyo alifikishwa mahakamani hapo jana na kurudishwa rumande, kwa kuwa mashitaka yanayomkabili, hayana dhamana. Alisomewa mashitaka mawili na Wakili wa Serikali, Leonard Chalo mbele ya Hakimu Mkazi, Hellen Riwa.
Wakili Chalo alidai Agosti 14 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Monyo alikamatwa akisafirisha gramu 1,512.65 za dawa za kulevya aina ya heroin. Alidai siku hiyo hiyo alikamatwa akiwa na gramu 3,477 za dawa hizo aina ya bangi.
Mshitakiwa hakuruhusiwa kujibu mashitaka ya kukutwa na dawa za kulevya, kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kuisikiliza. Kesi itatajwa Septemba 3 mwaka huu.
Profesa Mapesa ndani ya Banda la TIA Maonesho ya Wiki ya Kitaifa Elimu
,Tanga
-
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) Profesa Haruni Mapesa
akisaini Kitabu wakati alipotembelea Banda la TIA katika Wiki ya Elimu
Kita...
4 hours ago


No comments:
Post a Comment