Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, August 20, 2013

WAFUASI WA MUSLIM BROTHERHOOD WASHAMBULIA POLISI ASUBUHI HII NAKUUA POLISI 24, WAO WAFA 36

 Wafusi wa chama cha Muslim Bradherhood wakipambana na polisi nchini Misri
Polisi 24 wa Misri wameuawa huko Sinaii katika shambulio lilotokea leo asubuhi. Wakati huo huo Wizara ya mambo ya ndani nchini Misri imetowa taarifa za kuuawa kwa Wafuasi 36 wa chama cha Muslim Bradherhood ambao walikuwa wametiwa nguvuni wameuawa jana kwa bomu za kutowa machozi wakati waloipojaribu kutoroka pindi polisi ilipokuwa ikiwahamisha katika jela nyingine karibu na jiji la Cairo.Wizara hiyo ya mambo ya ndani nchini Misri imesema watu 36, ni wafuasi wa chama cha rais wa zamani aliepinduliwa na jeshi na kukamatwa Julay 3, ambapo vyombo vya usalam nchini humo vimesbabisha umwagaji wa damu mkubwa wakati wa kuwasambaratisha waandamanaji wanaoendelea kudai kurejeshwa madarakani mwa rais Mohamed Morsi.
Watu mia nane wamepoteza maisha nchibni Misri kwa kipindi cha siku tano, huku kiongozi wa kijeshi nchini humo akiapa kuendeleza mapambano dhidi ya waandamanaji.

Hayo yanajiri wakati wawakilishi wa nchi 28 za Umoja wa Ulaya wakitaraji kukutana leo jijini Bruxels kujadili kuhusu hali inayoendelea nchini Misri.


Kiongozi wa kijeshi jenerali Abdel Fattah al-Sissi ambaye amezungumza jana kwa mara ya kwanza tangu kutokea mauaji ya watu mia sita jumatano juma lililopita amesema kuwa jeshi halitovumilia hali yoyote ile ya vurugu na lipo tayari kupambana kwa kutumia nguvu kubwa ili kukomesha maandamano, bila hata hivo kujali kauli za viongozi wa magharibi wanaosema kuwa kunafanyika umwagaji wa damu.

Abdel Fattah al-Sissi
Jijini Bruxels mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya unafanyika, ikiw ani kikao cha kwanxza cha kidiplomasia cha hali ya juu kufanyika juu ya kuzungumzia hali ya nchini misri.
Jana Jumapili viongozi wa Umoja wa Ulaya, Herman Van Rompuy na jose Manuel Barroso wametahadharisha seriakli ya Misri kwamba Umoja wa Ulaya upo tayari kutathimini upya uhusiano wake na Misri iwapo haitositisha uwamgaji wa damu ambapo jukumu la kurejesha utulivu ni la jeshi na serikali.

Serikali nchini humo imewazikataza kamati za umma, zinazoundwa na makundi ya vijana wanaomiliki silaha ambao wamekuwa wakiwashambulia wale wote wanaoonekana kuwa ni wafuasi wa Muslim Bradherhood wanaofuga ndevu na wanawake wanaojisitiri kwa hijabu, pamoja pia na waandishi wa habari wa kigeni wanaotuhumiwa kumuunga mkono rais aliepinduliw amadarakani Mohamed Morsi. Baada ya kuwaacha vijana hao wakiendesha machafuko, hatimaye serikali hiyo hiyo imewatuhumu vijana hao kuendesha vitendo vilivyo kinyume cha sheria.

No comments:

Post a Comment