Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, September 26, 2013

MRISHO NGASA NOMA AWAONYESHA TFF JEURI YA FEDHA

Na Ezekiel Kitula
MSHAMBULIAJI Mrisho Ngassa wa Yanga, ameuambia uongozi wake yupo tayari ulilipe Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kitita cha Sh milioni 45 kutoka kwenye mshahara wake.
Ngassa amekubali kitita hicho cha fedha kitolewe kwa kuwa ana hamu ya kuanza kuitumikia Yanga baada ya kumaliza adhabu ya kutocheza mechi sita aliyopewa na TFF.
Imeelezwa Ngassa yupo tayari kukatwa katika mshahara wake na kuna taarifa katika Sh milioni 2 kila mwezi, atakatwa Sh 500,000.
Mshambuliaji huyo alisimamishwa mechi sita pamoja na kutakiwa kurudisha Sh milioni 30 alizolipwa na Simba pamoja na faini ya Sh milioni 15. TFF ilishikilia msimamo wake kwamba Ngassa hatacheza hadi atakapolipa fedha hizo za Simba.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa, Ngassa amekubali kuhusiana na hilo na alifikia makubaliano hayo na mwenyekiti, Yusuf Manji walipofanya kikao walipokutana jijini Mbeya, hivi karibuni.
Alipoulizwa kuhusiana na hilo jana, Ngassa alisema:  “Sawa, adhabu yangu ya kutocheza mechi sita za mashindano imemalizika, lakini siwezi kuongelea lolote, mimi ni mchezaji tu, kazi yangu ni ndani ya uwanja, hayo mengine ya kiutawala ni vyema yakatolewa ufafanuzi na viongozi,” alisema Ngassa.
Championi Jumatano lilimtafuta Manji ambaye alikiri kuzungumza na Ngassa kuhusiana na masuala kadhaa ya klabu yao likiwemo hilo.
“Mimi ni mwenyekiti, hakuna ubaya kuzungumza na Ngassa. Tunazungumza kwa ajili ya klabu yetu, hivyo msubiri akicheza mtamuona,” alisema Manji.
Taarifa nyingine zilieleza kuwa, Yanga ilikuwa tayari kupeleka fedha hizo leo, lakini ilitaka TFF wakate Sh milioni 45 katika Sh milioni 70 inazowadai na walikuwa katika mazungumzo katika hilo.
Kwa upande mwingine, Kocha Mkuu, Ernie Brandts, alisisitiza kwamba ana kila sababu ya kumpanga Ngassa kama atakuwa amerejea katika kikosi watakapoivaa Ruvu Shooting Jumamosi.
“Tuko naye kikosini kila siku, tunafanya naye mazoezi na tunashirikiana. Kama amerejea na yuko katika afya nzuri, nitampanga maana ninamhitaji,” alisema Brandts.
Wakati hilo la Ngassa linamalizika, taarifa nyingine za uhakika zimeeleza Manji alitarajia kukutana na kikosi kizima cha Yanga, jana usiku.
Mwenyekiti huyo alipanga kukutana na wachezaji na benchi la ufundi katika hoteli ya Serena jijini Dar ili kula chakula cha usiku na baadaye kujadili masuala kadhaa kikiwemo kipigo cha Azam FC na nini cha kufanya baada ya hapo ili kusonga mbele na ikiwezekana kutetea
-GP

No comments:

Post a Comment