Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, October 8, 2013

HUYU NDIYE BINTI ALIYENUSURIKA KATIKA AJALI YA BASI ILIYOUWA WANAMUZIKI WA BEND YA 5 STAR (ISSA KIJOTI) MWAKA 2011..!!



Tumemsikia Mwazani Said leo katika leo tena akituelezea namna alivyonusurika katika ajali ya gari iliyopelekea wasanii 13 ya band ya taarab ya 5stars kupoteza maisha.Ajali hiyo ilitokea tarehe 22 mwezi wa 3 mwaka 2011.Mwazani alisafiri na band kama mcheza show lakini yeye ilikuwa ni mara ya kwanza.Rafiki yake ambae alikufa kwenye band ndio alimwambia kuna kazi ya kucheza mikoani ambayo atatoka na pesa kidogo kuliko kukaa bure.
Wakasafiri na kuzuru mikoa mitano na yeye akafanya kazi yake ambayo alilipwa Tsh 100,000.Siku mbili kabla ya kurejea Dar wasanii waliopoteza maisha walikuwa wakiona vitu vya mauza uza.Msanii Issa Kijoti na mwimbaji mwingine wa kike walitokewa na mtu aliyevaa nguo nyeupe.Wakawaambia wenzao juu ya hilo wakawafanyia kisomo na dua ili waweze kukaa sawa.
Pia kulizuka ugomvi mkubwa ambao wasanii walikuwa wakigombana wao kwa wao mpaka Sheba Juma ambae ni marehemu alitaka kuondoka mwenyewe kurudi Dar.Lakini Ali J ambae yu hai alinusurika alisuluhisha ugomvi huo wakawa sawa.
Katika ajali hiyo wakiwa kwenye basi mwazani alikuwa amelala.Alikaa siti moja na marehemu Sheba Juma akamuomba wabadilishane siti ili yeye Mwazani alale maana alikuwa na usingizi.Alipolala alikuja kuzinduka baada ya siku 5 na kujikuta yupo hospital mkono umepooza na mguu umefanyiwa upasuaji na kuwekewa vyuma.Akamuuliza mama yake kumetokea nini mbona yupo hospital mama hakumjibu.Baba ndio akamletea gazeti akasoma na kuona kilichotokea na yule shosti wake aliyemuita wakacheze alipoteza maisha.


Baada ya ajali ile mpaka sasa mkono wake wa kushoto umepooza na mguu wa kushoto pia unavyuma bado.Walilipwa pesa ambazo yeye alizinunulia eneo kanyumba kadogo kakuishi.
 Wakati ananunua hapa sio yeye alikuja kununua.Kuna ndugu yake alikuja kupanunua lakini hakukuwa na choo.Ni mwaka sasa amekuwa akitumia choo cha jirani na kwa sasa amepigwa marufuku kutumia choo cha wenyewe.Baada ya kupigwa marufuku akarudi kwa baba yake ambae amepanga chumba na sebule.Baba na mama wanalala chumbani yeye analala sebuleni.
Sebule katika nyumba yake hiyo ambayo ipo Yombo dovya.
Huyu ndio jirani mwenye choo chake lakini amepigwa marufuku
Hapa ni chumbani kwake.
Kama ambavyo amesikika kwenye leo tena Mwazani anaomba kusaidiwa pesa ili aweze kujenga choo.Iwapo uliguswa na matatizo yake mchangie kwa namba 0759 789863 na 0657 795654.

No comments:

Post a Comment