Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikila Zenobi Lusale (65) Mkazi wa
Kijiji cha Sibwesa Tarafa ya Karema Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za
kumuuwa mjukuu wake kwa kumpiga na fimbo kichwani baada ya kumtuhumu
kumwibia debe moja la mahindi
Kwa
mijibu wa Kaimu kamanda wa polisi wa Mkoa wa Katavi Joseph
Shilinde tukio hilo lilitokea hapo jana majira ya saa kumi na moja
jioni katika kitongoji cha senta Magogo Kijiji cha Simbwesa Tarafa ya
Karema Wilayani hapa
Kaimu
kamanda Joseph Shilinde alimtaja aliyeuwawa kwa kupigwa na fimbo
kichwani na babu yake kuwa ni Stansilaus Joseph (15) Mkazi wa kijij
hicho
Siku
hiyo ya tukio mtuhumiwa Zenobi alikwenda kwa jirani kunywa pombe ya
kienyeji aina ya komoni mida ya mchana na kisha aliporejea nyumbani
kwake aliko kuwa akiishi na mjuu kuu wake huyo na ndipo alipo
mwita kwa lengo la maongezi
Marehemu
aliitika wito huo wa Babu yake kwa kujua wanataka kufanya
mazungumzo kama ambavyo wamekuwa wakifanya yeye na Babu yake mara kwa
mara
Kaimu
Kamanda alieleza kuwa ndipo mtuhumiwa alipoanza kumshutumu marehemu
mjukuu wake kuwa kuna mahindi debe moja yameibiwa ndani na yeye marehemu
ndiye aliyeiba mahindi hayo
Marehemu
baada ya kuambiwa tuhuma hizo alimkatalia katakata Babu yake kuwa yeye
haja iba mahindi hayo labda aliuza mwenyewe na amesahau kama
alimuuzia mtu kwani yeye hana tabia ya wizi
Mtuhumiwa
baada ya kujibiwa hivyo na marehemu alianza kumshambulia kwa fimbo
kichwani huku mjukuu wake huyo akipiga mayowe na ya kuomba msaada na
huku akimsihi babu yake asiendelee kumpiga lakini hakufanya hivyo
aliendelea kumpa kichapo tuu
Majirani
walifika katika eneo hilo na kumkuta mtuhumiwa akiwa ameshika fimbo
hiyo aliyotumia huku marehemu akiwa amegalagala chini na huku akiwa
ameishafariki dunia kutokana na kipigo hicho na majirani hao
walimkamata mtuhumiwa na kumweka chini ya ulinzi
Polisi
walifika kwenye eneo hilo na kumkuta mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi
wa wanakijiji hicho na ndipo walipomchukua hadi katika kituo cha polisi
cha Mpanda Mjini
Shilinde
alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi
maiti katika Hospital ya Wilaya hii na mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa
mahakamani mara uchunguzi wa tukio hili utakapo kuwa umekamilika
No comments:
Post a Comment