Rais wa
Nigeria, Goodluck Jonathan anaendelea kupokea matibabu mjini London
lakini wasaidizi wake wamesema kuwa hali yake sio mbaya sana.
Rais Goodluck alikwenda mjini London kwa mkutano , ingawa hakuweza kuhudhuria mkutano wenyewe.
Alisema
kuwa matibabu aliyokuwa anapokea rais huyo mwenye umri wa miaka 56 ni ya
kuzuia tu hali yake kuwa mbaya."tungependa kuwahakikishia kuwa Rais
Jonathan hayuko katika hali mbaya,'' alisema msaidizi wake Reuben Abati
Rais Jonathan amekuwa Rais tangu mwaka 2010, baada ya mtangulizi wake hayati Umar Yar Adua kufariki akiwa mamlakani.
Wakati huo alikuwa makamu wake wa Rais na hivyo kuchukua hatamu za uongozi.
Rais
alilazimika kuchelewesha siku yake ya kusoma bajeti, ya kila mwaka
bungeni baada ya toafuti kati ya serikali na bunge kuibuka.
Bwana
Jonathan pia anakumbwa na migawanyiko mikubwa chamani huku wapinzani
wake wakilumbania madaraka kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Pia anakabiliwa na wakati mgumu kupambana dhidi ya harakati za kundi la wapiganaji wa Boko Haram Kaskazini mwa Nigeria.
No comments:
Post a Comment