Jumuia
ya kimataifa imelaani vikali shambulio la kujitolea mhanga kwenye
mgahawa wa mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, ambao liliuwa watu kama 21 -
wengi wao wageni.
Waziri
wa mambo ya ndani wa Afghanistan, Mohammad Omar Daudzai, amesema
maafisa kadha wa serikali ya mitaa wamesimamishwa kazi na uchunguzi
unafanywa.
Kati
ya waliokufa ni afisa mkuu wa Shirika la Fedha la Dunia, IMF, nchini
Afghanistan, Wadel Abdallah, pamoja na wafanyakazi wanne wa Umoja wa
Mataifa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, amelaani shambulio hilo kuwa kitendo cha kutisha.
Mgahawa huo uko katika mtaa wa Kabul wa watu wanaojiweza na ukipendwa na wageni na maafisa wa serikali.
Taliban wamesema wamehusika na shambulio hilo.
Wageni 13 kutoka Marekani, Canada, Urusi, Libnan na Uingereza wameuwawa - na wengine ni raia wa Afghanistan.
Taarifa zinasema kuwa mshambuliaji alijilipua kwenye mlango wa mgahawa.
Baada ya mlipuko watu wawili waliwafyatulia risasi wateja.Chanzo BBC Swahili
No comments:
Post a Comment