Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, January 14, 2014

MAULID YA KUZALIWA BWANA MTUME (S.A.W) ILIYOFANYIKA HUKO ZANZIBAR


TA1A1112Maulid ya Hom yaliyosomwa na Vijana kutoka Mtendeni Mjini Unguja katika viwanja vya Mnazi mmoja jana, wakati wa Maulidi Matukufu ya kuzaliwa kwa Bwana Mtume (SA.W.) yanayofanika kila mwaka Kitaifa na kuhudhuriwa na Viongozi mbali mbali pamoja wananchi kutoa kila upende wa Nchi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A1143 Baadhi ya Viongozi wa Srikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na mashekhe waliohuduria katika Maulidi ya kuzaliwa Bwana Mtume (S.A.W.) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TUNAOMBA BOFYA HAPA NA ULIKE PAGE YETU KWA HABARI NYINGI(USIPITWEEEEEEEEEE)
TA1A1152 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Sheikh Sherali Champsi Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maulidi ya kuzaliwa Bwana Mtume (S.A.W.) alipowasili katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja  palipofanyika Maulid hayo jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A1162Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa na Viongozi wengine (kutoka kushoto) Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Mohamed Gharib Bilali,Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, na (kulia) makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamadi,wakiwa katika Maulidi ya kuzaliwa Bwana Mtume (S.A.W.) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A1163 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiteta jambo na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi  katika Maulidi ya kuzaliwa Bwana Mtume (S.A.W.) yaliyofanyika jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] TA1A1166 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa na Viongozi wengine wakisimama kumswalia Mtume (S.A.W.) wakati wa Maulidi ya Kusherehekea siku ya Kuzaliwa Bwana Mtume katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A1171Wake wa Viongozi na wanawake kutoka madarasa na vyuo mbali wakiongozwa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein wakiwa katika Viwanja vya Mnazi mmoja Mjini Unguja katika Maulid ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtuyme (S.A.W.).[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A1193 Wanafunzi wa Madrasatul Muntaha Kalam kutoka kijiji cha Ukongoroni  Wilaya ya kati,wakisoma Yarabiswali wakati wa Maulidi ya Kusherehekea siku ya Kuzaliwa Bwana Mtume (S.A.W.) katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A1218Wake wa Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakisimama kumswalia Mtume (S.A.W.) wakati wa Maulidi ya Kusherehekea siku ya Kuzaliwa kwake  Mtume katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

No comments:

Post a Comment