
“Ninawaagiza
wakandarasi wahakikishe wanarudi kwenye maeneo yao ya kazi mara moja,
kama Waziri Maghembe alivyoagiza. La sivyo Serikali itaangalia taratibu
na kuchukua hatua kali. Na mkandarasi atayekaidi hatapata kazi sio tu
Wizara ya Maji, bali Tanzania nzima”, alionya Naibu Waziri.
“Muwe
karibu na kuwahudumia vizuri wateja na kuwe na ratiba nzuri ya mgao na
ya kueleweka na kwenye dharura mfike mara moja bila kuchelewa. Muondoe
urasimu usio wa lazima katika kutoa huduma kwa wananchi wote”, alisema
Makalla.
Pia,
alisema wananchi waiunge mkono Serikali katika kutunza mazingira na
vyanzo vya maji na amekuja Wizara ya Maji kutimiza sera za maji na
mipango ya Serikali katika sekta hiyo na si vinginevyo. Na kuahidi
kuwasilisha maombi yote aliyoyapokea Wizarani na kuyapapa msukumo
yafanyiwe kazi, isipokuwa yale yaliyo ndani ya uwezo wao wafanye bidii
kuyatatua.
Naibu
Waziri Alhamisi aliendelea na ziara hiyo katika Halmashauri ya Wilaya
ya Mvomero na kukagua baadhi ya miradi ikiwemo Kibati, Kwadoli na
Kagugu. Vilevile, ametembelea bwawa la Mindu na kijijiji cha Lusungu.

Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala akimtwisha maji mama mara baada ya kufungua mradi wa maji Kagugu.
Naibu
Waziri wa Maji, Amos Makalla akizungumza na katika Ofisi za Mkuu wa
Mkoa Morogoro mara baada ya kuanza ziara yake Mkoani Morogoro, na kulia
ni Mkuu wa Morogoro, Joel Bendera.
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akiwa na mkandarasi katika kituo cha kusafishia maji cha Mifiga.
Kituo cha kusafishia maji cha Mmbogo kikiwa katika muendelezo wa ujenzi
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala akimtwisha maji mama mara baada ya kufungua mradi wa maji Kagugu.

No comments:
Post a Comment