Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, February 14, 2014

SIKU YA REDIO DUNIANI,HAKI YA USAWA WA KIJINSIA YAHIMIZWA

DSC_0019
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akisalimiana na Mkufunzi wa Redio za Jamii kutoka Unesco, Mama Rose Haji Mwalimu meza kuu wakati wa maadhimisho ya siku ya Redio Duniani yaliyofanyika Kitaifa mkoani Dodoma. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. Kajubi Mukajanga.
Amesema kwenye hotuba hiyo ya wakuu wa Umoja wa Mataifa kwamba hii ni fursa kwao wote, kusherehekea Siku Ya Radio Duniani kwa kuwatambua wanawake na kufanya yale yaliyo ndani ya uwezo wao kuzilea sauti mpya za kesho.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi Irina Bokova amesema na ninanukuu; Katika Siku ya Redio Duniani, tunaadhimisha chombo ambacho kinategemewa zaidi na watu wengi, wanaume kwa wanawake, duniani kote. Redio huwapa sauti wale wasio na sauti, husaidia kuelimisha watu wasio na elimu, na inaokoa maisha wakati wa majanga.
Akisoma taarifa hiyo amesema ikiwa ni chachu ya uhuru wa kujieleza na ushirikishwaji wa wengi, redio ni muhimu katika kujenga jamii yenye uelewa na kukuza heshima na uelewano baina ya watu. 

Mama Rose Edited (3)

No comments:

Post a Comment