Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, February 14, 2014

YANGA YAWASILI COMORO,WAANZA MAZOEZI


Wachezaji wa Young Africans wakifanya mazoezi leo jioni katika uwanja mdogo uliopo katika Hotel ya Retaj -Moroni
Kikosi cha Young Africans kimewasili tayari kimewasili salama katika Visiwa vya Comoro majira ya saa 6 kamili mchana kwa shirika la ndege la Precison Air na kupokelewa na wenyeji wao kisha moja kwa moja kuelekea katika hotel ya Retaj Moroni ambapo ndipo msafara wa watu 30 ulipofikia.
Mara baada ya kuwasili Uwanja wa ndege mvua kubwa iliyoambatana na upepo ilinyesha hali iliyopelekea pia timu kuchelewa kutoka Uwanja wa ndege kuelekea Hoteli ambapo timu ilifika Ratej hoteli majira ya saa 9 mchana.
Kocha mkuu wa Young Africans jioni amekiongoza kikosi chake kufanya mazoezi mepesi katika uwanja mdogo uliopo hotelini kutokana na mvua na umbali wa kwenda mji wa Mitsamihuli ambapo ndipo kuna uwanja utakaotumika kwa ajili ya mchezo siku ya jumamosi.
Hali ya wachezaji wote ni safi na hakuna majeruhi hata mmoja kuelekea kwenye mchezo huo, ambapo kesho asubuhi majira ya saa 4 kikosi cha Young Africans kitafanya mazoezi mepesi katika Uwanja wa Said Mohamed Cheick Mitsamihuli kwa ajili ya mchezo utakaofanyika siku ya jumamosi majira ya 9 kamili kwa saa za Visiwa vya Comoro.
 TUNAOMBA BOFYA HAPA NA ULIKE PAGE YETU KWA HABARI NYINGI MOTOMOTO(USIPITWEEEE)

No comments:

Post a Comment