Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, March 20, 2014

AJALI::LORI LAGONGA PIKIPIKI MAENEO YA SINZA

 Pikipiki 'bodaboda' ikiwa imekanyagwa na tairi la Scania.
AJALI hii imetokea jioni ya leo eneo la Sinza-Palestina, Dar baada ya lori aina ya Scania lenye namba za usajili T303 ABV kuigonga pikipiki inayotumika kubeba abiria maarufu kwa jina la bodaboda.
Gari aina ya Scania likionekana kwa mbele likiwa limesimama baada ya ajali hiyo kutokea.
Ajali hiyo iliwashangaza watu waliokuwepo karibu na eneo hilo kwani ilikuwa ni ya kushtukiza ambayo ilimwacha kila mtu mdomo wazi. Hakuna mtu aliyejeruhiwa katika ajali hiyo japokuwa pikipiki iliharibika vibaya.


 
Bodaboda ikiwa nyang'anyang'a baada ya kukanyagwa na Scania.

SOURCE: GPL

No comments:

Post a Comment