MASHINDANO MAKUBWA YA KLABU BARANI AFRIKA, CAF CHAMPIONZ LIGI, IJUMAA YANAINGIA RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16 ILI KUPATA TIMU 8 AMBAZO ZITAINGIA KWENYE DROO KUPANGA MAKUNDI MAWILI YA TIMU 4 KILA MOJA.
Mabingwa
Watetezi, Al Ahly ya Misri, ambao Raundi iliyopita waliwatoa Mabingwa
wa Tanzania Bara, Yanga, kwa Mikwaju ya Penati baada kwenda Sare ya
Jumla ya Bao 1-1 katika Mechi mbili, wataanza kucheza Ugenini huko Libya
na Klabu ya Al Ahli – Benghazi.
Nao TP Mazembe ya Congo DR,
Klabu yenye Mastraika wawili Mashujaa wa Tanzania, Thomas Ulimwengu na
Mbwana Samatta, itakuwa Ugenini huko Ivory Coast kucheza na Sewe Sport.
Mechi nyingine zenye mvuto ni ile kati ya Nkana FC ya Zambia na Magwiji wa Egypt, Al Zamalek itakayochezwa huko Zambia..
Klabu nyingine ya Congo DR ni AS Vita ambayo itakuwa Nyumbani kucheza na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.
Marudiano ya Mechi ya Raundi hii ni Wikiendi ya Machi 28.
CAF CHAMPIONZ LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
Ijumaa Machi 21
16:00 Al Ahli - Benghazi – Libya v Al Ahly - Egypt
16:00 Nkana FC – Zambia v Al Zamalek - Egypt
19:30 AS Bamako – Mali v Espérance Sportive de Tunis – Tunisia
Jumapili Machi 23
16:30 AS Vita Club - Congo, DR v Kaizer Chiefs - South Africa
16:50 AC Leopards de Dolisie – Congo v Al-Hilal - Sudan
19:00 Sewe Sport - Ivory Coast v TP Mazembe - Congo, DR
19:30 Horoya Athlétique Club – Guinea v Club Sportif Sfaxien - Tunisia
21:15 Entente Sportive de Sétif - Algeria v Coton Sport FC - Cameroon
No comments:
Post a Comment