Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, March 13, 2014

YANGA YAWAFUATA MTIBWA MOROGORO

Young Africans wakisalimiana na wachezaji wa timu ya Flumurtari
Msafara wa Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Young Africans leo asubuhi umeondoka jijini Dar es salaam kuelekea mjini Morogoro tayari kwa mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar siku ya jumamosi, mechi itakayopigwa kwenye dimba la Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Young Africans inayonolewa na makocha Hans Van der Pluijm kutoka Uholanzi, Charles Mkwasa na Juma Pondamali wazawa jana jioni ilifanya mazoezi katika Uwanja wa Kaunda ikiwa ni masaa 10 baada ya kuwasili kutokea jijini Cairo ilipocheza dhidi ya Al Ahly katika mashindano ya Klabu Bingwa barani Afrika.
Kuhusu mchezo wenyewe Kocha Hans amesema haifahamu vizuri timu ya Mtibwa Sugar lakini kwa kushirikiana na wenzake wamejiandaa kuhakikisha timu inafanya vizuri na kupata pointi 3 katika mchezo huo, yaliyotokea Misri yameshapita sasa kilichobakia ni kutetea Ubingwa wa Ligi Kuu. 

Kwa mujibu wa daktari wa timu ya Young Africans Dr Suphian Juma amesema wachezaji wote wapo fit kuelekea kwenye mchezo huo na mchezaji pekee atakayekosena ni Mrisho Ngasa ambaye alipata maumivu ya nyama za paja hivyo kwa sasa bado anaendelea na matibabu huenda akaanza mazoezi na wenzake mwishoni mwa wiki hii. 
Mechi dhidi ya Mtibwa Sugar siku ya jumamosi itafungua ukurasa mzuri kwa Young Africans kwani endapo itashinda mchezo huo itarejea kwenye kiti cha uongozi wa Ligi Kuu na kujitengenezea mazingira mazuri ya kutetea Ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo. 
Msafara umeondoka ukiwa na idadi ya watu 31 wakiwemo wachezaji 22 pamoja na benchi la Ufundi ambapo leo jioni timu inatarajiwa kufanya mazoezi mjini Morogoro kabla ya kesho kufanya mazoezi mepesi ya mwisho kuelekea siku ya mechi.
Wachezajii waliondoka ni:
Walinda Mlango: Deo Munish "Dida", Juma Kaseja na All Mustafa "Barthez"
Walinzi: Juma Abdul, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, David Luhende, Nadir Haroub "Cannavaro", Kelvin Yondani na Ibrahim Job
Viungo: Frank Domayo, Athumani Idd "Chuji",  Nizar Khalfani, Hassan Dilunga na Haruna Niyonzima
Washambuliaji: Saimon Msuva, Said Bahanuzi, Hamis Kizza, Emmanuel Okwi, Didier Kavumbagu, Hussein Javu na Jerson Tegete

No comments:

Post a Comment