Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, April 1, 2014

MOYES AMUONYA MWAMUZI CARBALLO JUU YA KUJIRUSHA KWA ROBBEN MAN UTD IKIIVAA BAYERN LEO OLD TRAFFORD!!

KOCHA  Mkuu wa Mashetani wekundu, Manchester United, David Moyes amemuambia mwamuzi  wa Hispania, Carlos Carballo kutoa maamuzi sahihi katika mchezo wao dhidi ya mabingwa wa Ulaya na Bundesliga, Bayern Munich kutokana na tabia ya wachezaji wa timu hiyo kujiangusha.
Man United inakabilina na  Bayern usiku wa leo uwanja wa Old Trafford katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali, Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Bayern inapewa nafasi kubwa ya kushinda, lakini timu hiyo ya kocha Pep Guardiola ilishutumiwa baada ya kuitoa Arsenal katika raundi iliyopita, huku  kocha wa washika bunduki wa London, Arsene Wenger akimlaumu Arjen Robben kuwa  ni hodari wa kujirusha kujiangusha.
Moyes alisema: “Tunawaamini marefa watafanya uamuzi sahihi. Kujirusha ni moja ya vitu vibaya vya kufanyia kazi. Ningependa kutahadharisha juu ya hilo, lakini nisingependa kumlenga mchezaji binafsi,”.
Winga Mholanzi Anayepaa: Nyota wa Bayern, Arjen Robben amekuwa akishutumiwa kwa kujiangusha kirahisi
Wishlist: Manchester United boss David Moyes hopes referee Carlos Velasco Carballo punishes diving
Angalizo la tahadhari: Kocha wa Manchester United, David Moyes anatumai refa Carlos Velasco Carballo atwaadhibu wachezaji wa kujiangusha,NA BARAKA MPENJA

BOFYA HAPA NA ULIKE PAGE YETU KWA HABARI NYINGI ZA KUSISIMUA

No comments:

Post a Comment