Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, April 1, 2014

Sitta ampa barua Mtikila aende kwa JK

 

Mwenyekiti wa Bunge la Katiba,Samuel Sitta.PICHA|MAKTABA
“Sitakwenda kumuona Kikwete, bali ninajua kwamba tukishindwa kuipata Tanganyika kwenye Bunge hili nitakwenda mahakama za kimataifa,” alisema Mtikila ambaye amekuwa akihubiri Utanganyika tangu nchi ilipoingia kwenye siasa za vyama vingi mwanzoni mwa miaka ya tisini.
Alisema kwa sasa anasubiri kumaliza majadiliano juu ya sura ya kwanza na ya sita ya rasimu ya katiba kuona mwelekeo na suala la muundo wa Muungano kuwa wa serikali tatu litakwamishwa, ataondoka Dodoma na kurejea Dar es Salaam kuandaa kesi.
Hoja kubwa katika mchakato wa kutunga Katiba mpya iko kwenye muundo wa Muungano baada ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwasilisha rasimu inayoonyesha kuwa wengine wanataka muundo wa Muungano wa serikali tatu, jambo ambalo linaonekana kupingwa na wajumbe kutoka chama tawala cha CCM.
Bunge hilo linaundwa na wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wawakilishi wa Baraza la wawakilishi wa Zanzibar na wawakilishi wa makundi mbalimbali wapatao 201 ambao walitangazwa na Rais Kikwete.
Lakini Mchungaji Mtikila anapingana na muundo wa Bunge la Katiba.
“Nitakwenda mahakamani kupinga sheria yote ya Mabadiliko ya Katiba kwani waliopaswa kushiriki Bunge la Katiba ni wajumbe waliochaguliwa na wananchi kwa ajili ya Bunge la Katiba, na siyo hawa wabunge na wengine wa kuteuliwa,” alisema.
Hoja ya Mtikila
Pamoja na mambo mengine katika hoja yake, Mtikila analalamika kuwa amezuiwa kuchangia katika Bunge hilo baada ya kuandikiwa barua na Ofisi ya Bunge.
Hata hivyo, katibu wa Bunge la Katiba, Yahya Khamis Hamad alisema: “Hili kwangu ni jipya na sidhani kuwa linawezekana.”
Mtikila alisisitiza kuwa alipewa barua hiyo Jumatano iliyopita ikiwa ni majibu ya barua yake aliyoiandika kwa ofisi hiyo wiki iliyopita.
“Nilianza kuhisi baada ya kuona ninanyimwa kuchangia; nikaandika barua kuomba maelezo kwa nini ninakosa nafasi ya kuchangia bungeni,” alisema na kuongeza:
“Lakini juzi nilipokea barua kutoka kwa katibu wa Bunge ikinikataza kuchangia tena bungeni kutokana na kauli zangu za kukosoa mchakato.”chanzo Mwanainchi



No comments:

Post a Comment