Katika hali isiyokuwa kawaida train ya abiria ilokuwa imeanza safari yake saa nane kasoro mchana wa leo kutoka jijini kuelekea mkoani Mbeya imelazamika kugeuzia njiani kurudi pale kituoni TAZARA na itaendelea na safari saa kumi na moja na nusu jioni ya leo.
Sababu waloelezwa abiria inaitwa (SABABU ISIYOZUILIKA).
Wote mlowasindikiza ndugu jamaa na marafiki jueni kwamba bado wapo hapa hapa jijini Dar mpaka sababu hiyo itapotengamaa.
Pia wadau msishangae siku utapoenda pale TAZARA kumpokea mgeni wako itakubidi ulipe kiingilio cha shilingi elfu moja.
Kiasi hiki kipya kimepandishwa baada ya kile cha mia 5 cha awali.Kiwango hiki ni kikubwa sana kwa watu wa maisha ya chini wanaokuja kupokea ndugu zao.
CDF JACOB MKUNDA AWAFIVISHA NISHANI MAJENERALI NA MAAFISA WA JWTZ
-
MKUU wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John
Mkunda kwa niaba ya Mhe Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan
amewav...
1 hour ago
No comments:
Post a Comment