Divock Origi (kulia) amesafiri mpaka Liverpool kujadili
uwezekano wa kujiunga na klabu hiyo.
Liverpool wanakaribia kukamilisha usajili wa wachezaji
wawili, nyota wa Ubelgiji katika fainali za kombe la dunia mwaka huu, Divock
Origi na winga wa Benfica, Lazar
Markovic.
Usajili huo utaigharimu Liverpool dau la paundi milioni 30.
Orig alipigwa picha akiwasili mjini Liverpool jana jumatano
ili kuzungumza na maofisa wa klabu katika uwanjani wa mazoezi wa Melwood na
anaweza kupimwa afya leo alhamisi.
Ada ya uhamisho ya paundi milioni 19.8 kwa ajili ya Markovic
inaaminika imeshakubaliwa na Benfica, wakati Origi anaonekana ataigharimu
Liverpool paundi milioni 10 kutokea klabu ya Lille ya Ufaransa,.
Hata hivyo, nao Tottenham waliripotiwa kuiwinda saini ya
nyota huyo
Origi (pichani mwenye nguo yenye rangi ya njano)
alichukuliwa kwenda uwanja wa mazoezi wa Liverpool, Melwood



No comments:
Post a Comment