Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, August 20, 2014

ROJO ATUA MAN UNITED KUKAMILISHA USAJILI

Amewasili: Marcos Rojo amewasili England leo kwa ajili ya kukamilisha usajili wake Manchester United.
KLABU ya Manchester United imekubali kutoa Pauni Milioni 16 kumnunua beki wa Sporting Lisbon, Marcos Rojo.Rojo, ambaye ametua mjini Manchester leo na kusema kuhamia United ‘anahisi kama ndoto’, anatarajiwa kusaini Mkataba wa miaka minne akifaulu vipimo vya afya

 
na kukubali vipengele binafsi vya kandarasi yake.Louis van Gaal ametoa kipaumbele kwa usajili wa beki huyo mtumia mguu wa kushoto, Rojo, mwenye umri wa miaka 24, kufuatia kufungwa mabao 2-1 katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya England Jumamois na Swansea.
Winga Luis Nani, aliyejiunga na United kutoka Sporting kwa Pauni Milioni 17 mwaka 2007, amerejeshwa kwa mkopo klabu yake hiyo ya zamani, ilia ni sehemu ya dili hilo la Rojo

No comments:

Post a Comment