Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, December 14, 2014

AIBU KUBWA::MCHUNGAJI JOHN PAUL ANASWA NA WANAWAKE WATATU GEST

Pastor John Paul Simon Rubanguka wa kanisa la kiroho la Maximum Deliverance lililopo Masaki, Dar ambaye alinaswa akichezewa utupu na wanawake watatu ambao ni kama waumini wake kwa sababu wote ni Wakristo.Pasta John Paul Simon Rubanguka wa kanisa la kiroho la Maximum Deliverance lililopo Masaki, Dar baada ya kunaswa na wanawake watatu wakimchezea utupu.
OFM YATONYWA UCHAFU WA PASTOR
Ilikuwa Jumanne ya Aprili Mosi, 2014, saa 4:14 asubuhi, chanzo cha habari kilipiga simu chumba cha habari cha Global na kuwataka makachero wa OFM ambapo alipounganishwa nao alisema:

“Jamani kama kweli hapo ni OFM nina malalamiko. Mimi nimeshtukia mchezo mchafu unaotaka kufanywa na pastor (mchungaji) mmoja anaitwa Rubanguka.
Pasta John Paul Simon Rubanguka akijaribu kujitetea.
“Huyu pastor amempa dili dada mmoja kumtafutia wasichana wazuri watatu na kuwapeleka kwenye nyumba moja hivi kisha wawe wanamchezea utupu wake huku wao wakiwa kama walivyozaliwa, ndiyo furaha yake ilipo. Wasichana wameshapatikana.”
Makamanda wa Polisi wakimbananisha na kumtuliza Pasta huyo ili apunguze munkari.
MSHIKO WA NGUVU NA SAFARI JUU
Mtoa habari huyo aliendelea kudai kuwa, pastor huyo alisema wasichana watakaokuwa wakichezea utupu atawafanyia usaili wa kwenda kuwauza kwenye kasino moja iliyopo Uarabuni ambayo yeye ni wakala wa kuwapelekea malaya huko.
Pastor akiwa na mmoja wa wanawake waliofumaniwa naye.
Chanzo hicho kiliendelea kudai kuwa, pastor huyo aliwaahidi wanawake hao kitita cha shilingi 300,000 kila mmoja kwa wale watakaofaulu kumchezea vizuri, sanjari na kuwakatia hati za kusafiria ‘passport’.


Makamanda wa OFM wakimtuliza Pasta.
OFM YAWEKA MTEGO
Baada ya kupata ishu nzima, OFM ilifanya ukachero na kugundua mahali ambapo tukio hilo lilipangwa kufanyika, ni kwenye danguro moja lililopo Kinondoni jijini Dar.
Wanawake walionaswa katika tukio hilo wakivaa viwalo vyao.
OFM ilifika kwenye nyumba hiyo na kufanya ushushushu wake ambapo walifanikiwa kuweka mitambo yao sambamba na kulishirikisha jeshi la polisi kwa ajili ya kumnasa mtumishi huyo wa Mungu akifanya vitendo hivyo.
Saa 8:11 mchana, OFM wakiwa wamejibanza eneo hilo waliwashuhudia warembo watatu, weupe wakielekea kwenye nyumba ambayo mtoa habari wetu aliielekeza.
Kitambulisho cha Pasta.
PASTOR AWASILI KWA MBWEMBWE
Saa 11:23 jioni, OFM wakiwa hawajaanza hata kujisikia kuchoka, walimwona pastor huyo akiwasili kwa mbwembwe akiwa ndani ya gari dogo na kugeuza kwa staili ya kupiga ‘norinda’ kisha akashuka. Mkononi alishika maji makubwa. Alipokelewa na mmoja wa wanawake hao.
Bango lililopo Kinondoni Mkwajuni, Dar likieleza lilipo kanisa la Pasta huyo.
MCHEZO WAANZA
Saa 11:40 jioni, makachero wa OFM walifanya uchunguzi wa kina na kubaini kuwa, tayari mchezo ulishaanza ambapo waliwataarifu polisi na kuungana nao kwenda kuvamia nyumba hiyo.
Msafara wa OFM na polisi hao ulifika nje ya chumba kilichokuwa kikidaiwa kufanyika uchafu huo. Sauti ya muziki na wanawake waliokuwa kama wapo kwenye darasa la siri zilisikika.
Polisi waligonga mlango na kujitambulisha kisha wakaomba wafunguliwe mlango haraka ndani ya sekunde chache.
PASTOR APATA MCHECHETO
Pasta John na wanawake hao walitii amri kwa kufungua mlango ambapo mchungaji huyo alikumbwa na mchecheto na kutaka kurukia juu ya dari lakini polisi walimtafadhalisha kutulia pamoja na wanawake hao kama walivyo.
OFM ikiwa chumbani humo iliwashuhudia wanawake hao wakiwa watupu mbele ya pastor huyo ambapo walikuwa wakimnengulia viuno.
Baada ya kupewa kibano, warembo hao walimwanika pastor huyo kwamba ndiye aliyewatuma wamchezee wakiwa watupu ili awalipe shilingi laki tatu kila mmoja, pia kuwapeleka Uarabuni kwenye kasino.
UTETEZI WA PASTOR
Kwa upande wake, Pastor John alijitetea kuwa anaomba asamehewe kwa gharama zozote ili taarifa hizo zisifike popote kwani ishu hiyo ilikuwa si amri yake bali shetani alimpitia.
“Jamani naomba tumalize humuhumu ndani, mnajua mimi ni Pastor wa Kanisa la Maximum Deliverance, sasa ukweli ni kwamba waumini wangu hawatanielewa, chondechonde ilindieni kazi yangu jamani,” alijitetea.
Mpaka OFM inaondoka eneo la tukio, pastor huyo na wanawake ‘wake’ walikuwa kwenye harakati za kupelekwa mbele ya vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua zinazostahili.
KUTOKA MEZANI KWA MHARIRI
Siku zote kazi ya OFM ni kuwajibikia matendo maovu na si kuwaonea watu  kwa lengo la kuwachafua. OFM inapopata habari huichunguza ukweli wake kwanza kabla ya kuchukua hatua ya kuifanyia kazi moja kwa moja, yaani kufika kwenye eneo la tukio.
Lengo kubwa la kutoa habari za aina hii ni kuwakumbusha watu namna ya kuishi maisha yanayompendeza  Mungu. Wengi wamebadilika, sasa wanaishi vizuri wakiwa watu wapya na wanyenyekevu pia wenye kufundisha wenzao.
-GPL

No comments:

Post a Comment