Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, December 19, 2014

DKT. BILAL AMTUNUKU SHAHADA YA UZAMIVU, RAIS KIKWETE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimtunuku shahada ya heshima ya Uzamivu (PhD) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kutambua mchango wake katika Jamii, kitaifa na kimataifa pamoja na kufanikisha kuanzishwa kwa Taasisi hiyo. Dkt Jakaya alitunukiwa Shahada hiyo wakati wa Mahafali ya pili ya Taasisi hiyo yaliyofanyika leo Jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae pia ni Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimtunuku shahada ya Sayansi Uhandisi na Hesabu PhD, James Philip, wakati wa Mahafali ya 2 ya Taasisi hiyo iliyofanyika leo jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia kwenye Mahafali ya 2 ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliyofanyika leo jijini Arusha.


Baadhi ya wahitimu...
Baadhi ya wahitimu...
Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake ambaye ni Mkuu wa Taasisi hiyo, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu.
Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake ambaye ni Mkuu wa Taasisi hiyo, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika maandamano na viongozi wa Taasisi hiyo pamoja na wahitimu, wakati wa Mahafali ya 2 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika leo jijini Arusha. Picha na OMR

No comments:

Post a Comment