Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, December 11, 2014

Makamu wa Rais wa JICA amtembelea Waziri wa Ujenzi Ofisi kwake Jijini Dar es Salaam


 Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan JICA, Kato Hiroshi  akimueleza jambo Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo Sekta ya Ujenzi wa barabara nchini wakati alipomtembelea Ofisini kwake  jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akifafanua jambo kwa Makamu wa Rais wa JICA Kato Hiroshi.
 Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Gerson Lwenge ( wapili kulia), akimuuliza  swali  Makamu wa Rais wa JICA Kato Hiroshi  (wa kwanza kushoto) kuhusu miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Serikali ya Japan kupitia Shirika  hilo la Maendeleo.


 Baadhi ya wajumbe  kutoka  JICA wakiangalia baadhi ya picha za matukio mbalimbali katika Wizara ya Ujenzi kabla ya mkutano wao na Waziri wa Ujenzi.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makamu wa Rais wa JICA, Kato Hiroshi  mara baada ya kumaliza mkutano wao uliofanyika Wizara ya Ujenzi.


PICHA ZOTE KWA HISANI YA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI, WIZARA YA UJENZI.

No comments:

Post a Comment