Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, December 9, 2014

UTAFITI: WANAUME HAWAOI KAMWE AINA HIZI KUMI ZA WANAWAKE (UTAISHIA KUITWA GIRLFRIEND SIO MKE)



1.Mwanamke anaelaumu kwa kila kitu (The Complaint Box), hata umfanyie zuri lipi bado atalaumu. Huona mabaya tu, hana zuri kwake.

2.Mwanamke anayejiona amekamilika, anajihisi anaweza kufanya lolote bila mwanaume, na kuhisi anaweza kufanya lolote analofanya mwanaume, daima anataka haki sawa na hana muda wa kumheshimu mwenza wake.


3.“The Crybaby” Huyu silaha yake ni machozi tu saa zote. Hana namna nyingine ya kuelezea matatizo yake zaidi ya kulia. Muda wote anataka kuonewa huruma, kubembelezwa masaa 24, hana furaha muda wote! Mwanaume huona bora asioe kuliko kuoa mwanamke mwenye sifa hizi.


4.Mzuri Usoni, Muonekano mzuri, ila kichwani hamna kitu (The Bimbo) mwanamke wa aina hii hujali tu muonekano wake, na hiyo ndio silaha yake na kujiona malaika! Hana mipango yoyote kimaisha. Japo wanaume wanapenda wanawake wenye muonekano mzuri, kuna muda huhitaji mwanamke anyeweza kupanga nae maisha.





5.Haachi Utoto, na kutotaka kuwa mtu mzima. Sio kila mwanaume anapenda jukumu la malezi kwa mpenzi wake! Japokuwa kuna kipindi mwanaume anaweza kupenda tabia hiyo, ila baadae huchoka kuwa “baba” na kuhitaji kuwa mpenzi na hapo ndipo shida huibuka.

6.Mwanamke Mbinafsi. Daima anataka afanyiwe mazuri yote yeye tu, Mchoyo na hapendi ndugu wa mpenzi wake, pia hayuko tayari kuona mpenzi wake anamsaidia mtu mwingine!


7.Mwanamke anayehisi anawajua wanaume kupita kawaida. Aina hii ya wanawake huhisi wanadanganywa muda wote, hawana muda wa kuwa serious na mahusiano kwa kuhisi wataumizwa kwa kuwa eti “Wanaume wote ni sawa”


8.Mwanamke anaeongea kupita kiasi! Hutaka kumwambia mpenzi wake kila kinachofanywa na watu wengine (Mmbea) hatulii, na mara kadhaa humtia aibu mpenzi wake kwa kuongea ujinga sehemu pasipofaa.


9.Mwanamke anayeishi Maisha ya Kusadikika, Maisha ya ndoto, na Maisha yanayoonekana kwenye tamthilia za mapenzi tu! Huhitaji kuishi maisha yaliyokamilika, na kutaka kila zuri analoliona kwa mwanaume yoyote, basi na mpenzi wake awe nalo!


10.Yote tisa, Kumi ni “Gold digger” Mwanamke anayejali zaidi pesa kuliku utu! Aina hii ya wanawake huwa na mtu kwa kuwa anakipato tu, siku ukikosa basi hata salamu hupati. Humuuliza mpenzi wake juu ya kipato chake, ana kiasi gani bank, nk. Hayuko upande wa mpenzi wake akikwama, kuumwa, kufiwa nk, badala yake na yeye hutengeneza tatizo lake mfano kuumwa nk.

No comments:

Post a Comment