Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, January 13, 2015

KATUNI YA MTUME MUHAMMAD KUCHAPISHWA KESHO

Gazeti la Vibonzo la Charlie Hebdo.
 Gazeti la kila wiki la vibonzo la Charlie Hebdo la Ufaransa toleo la kesho Jumatano linatarajiwa kuchapisha kibonzo cha Mtume Muhammad katika ukurasa wake wa mbele chini ya kichwa cha habari "Yote yameshasamehewa"
 Walioona kibonzo hicho wanasema Mtume Muhammad ataonekana akishikilia bango lililoandikwa "Je suis Charlie" maneno yenye tafsiri "Mimi ni Charlie, yaliyotumika kuonyesha mshikamano, baada ya shambulizi katika ofisi za gazeti hilo Jumatano wiki iliyopita ambapo wafanyakazi kumi na wawili wa gazeti hilo waliuawa.


Nakala milioni tatu za gazeti hilo la kesho tayari zimeshachapishwa tofauti na kawaida ambapo huwa linachapisha nakala sitini elfu kwa wiki.


(CHANZO: BBC SWAHILI)

No comments:

Post a Comment