Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, July 23, 2015

KAGAME CUP::YANGA WALEEEE WAJITUNGULIA TELECOM GOLI 3

Mshambuliaji wa Yanga Malimi Busungu akishangilia goli lake
Mshambuliaji mpya aliyesajiliwa na klabu ya Yanga akitokea Mgambo JKT ya Tanga, Malimi Busungu,  amefanikiwa kufunga magoli mawili kati ya matatu wakati Yanga ikicheza dhidi ya Telecom ya Djibouti kwenye mchezo wa Kundi A michuano ya Kagame Cup na kuifanya Yanga kuandika ushindi wa kwanza kwenye michuano hiyo inayozidi kuchukua sura mpya.
Busungu alianza kufunga goli la kwanza dakika ya 26 kipindi cha kwanza bada ya mashambulizi kadhaa hatimaye akafanikiwa kuukwambisha mpira kambani. 
Kitu kilichowashangaza mashabikim wengi wa Yanga ni pale timu hiyo ilipopata penati mbili lakini wapigaji walishindwa kutumia nafasi hizo kufunga magoli.
Haruna Niyonzima akimtoka mlinzi wa Telecom Warsama Ibrahim Aden
Amis Tambwe alikosa penati ya kwanza dakika ya 36 baada ya Simon Msuva kuangushwa kwenye eneo la hatari lakini Tambwe alipiga mpira nje. Dakika ya 45 Yanga ilipata penati baada ya mlini wa Telecom kuunawa mpira kwenye eneo la hatari lakini Simon Msuva mfungaji bora na mchezaji bora wa ligi 

 
msimu uliopita penati yake ilipanguiliwa na golikipa wa Telecom Nzokira Jeef.
Kipindi cha kwanza kilimalizika Yanga wakiwa mbele kwa goli 1-0 kitu ambacho kiliwashangaza wengi kwasababu walikuwa wakiamini Telecom ni timu dhaifu kutokana na kufungwa goli 5-0 na Khartoum ya Sudan.
Wachezaji wa Yanga wakimpongeza Malimi Busungu baada ya kufunga goli la kwanza
Kipindi cha pili kocha wa Yanga Van Pluijm alifanya mabadiliko kwa kumtoa Simon Msuva na nafasi yake ikachukuliwa na Godfrey Mwashiuya wakati Amis Tambwe nafasi yake ilichukuliwa na Kpah Sherman na Deus Kaseke alitolewa kumpisha Andrey Coutinho.
Dakika ya 68 Busungu alifunga goli la pili kabla ya Mwashiuya hajamalizia bao la tatu na lamwisho dakika ya 74 akipiga shuti kali lililogonga mtambaa panya kisha kumgonga mlinda mlango na kutinga nyavuni.
Baada ya mchezo kumalizika, Malimi Busungu alaitangazwa kuwa nyota wa mchezo huo na kukabidhiwa king’amuzi na kituo cha television cha DSTV.
Kwa matokeo hayo, Gor Mahia wanaendelea kuongoza kundi A wakiwa na pointi 6, wakifuatiwa na Khartoum ambayo inapointi sita pia lakini wanatofautiana magoli ya kufunga na kufungwa. Yanga wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi tatu sawa na KMKM lakini nao wanatofautihwa kwa magoli na Telecom ndio wanashika mkia kwenye kundi hilo wakiwa hawajapata ponti hata moja.

No comments:

Post a Comment