Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, August 12, 2015

MAJIMBO MATANO KURUDIA UCHAGUZI KURA ZA MAONI CCM

Nape Nnauye akizungumza kwenye moja ya mikutano na waandishi wa habari
KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi(CC) imeagiza kurudiwa kwa uchaguzi katika majimbo matano kutokana na dosari mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa kura ya maoni.
Majimbo hayo ni Makete,Busega,Ukonga,Rufiji na Kilolo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Dodoma Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye amesema mchakato huo utarudiwa siku ya alhamisi Agosti 13.
Amesema baada ya uchaguzi huo matokeo yatapelekwa katika vikao vinavyoendelea kwa ajili ya uamuzi.
Akizungumzia kuhusu vikao vinavyoendelea Ndugu Nape amesema vikao hivyo vinaendelea vizuri ambapo jana kikao cha kamati ya maadili kiliendelea mpaka usiku.

Amesema leo wanatarajia kumaliza kikao cha CC ambapo kesho na kesho kutwa watamaliza na kikao cha halmashauri kuu ya chama hicho(NEC) kama ilivyopangwa

No comments:

Post a Comment